Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) likishirkiana na Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii (ESRF) limefanya uzinduzi wa Ripoti ya Maendeleo ya Afrika 2016 ambayo imekuwa na kauli mbiu ya Kuongeza Kasi ya Kuweka Usawa wa Kijinsia na Kuwawezesha Wanawake.

Akizungumza kwa niaba ya Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa, Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Awa Dabo alisema kuwa ripoti hiyo inaonyesha jinsi gani watu wanaoishi Afrika wanapiga hatua kupata maendeleo lakini wakikabiliwa na changamoto usawa wa kijinsia na uwezeshaji kwa wanawake.

"Kupitia ripoti hii UNDP inaonyesha jinsi gani watu wanaoishi Afrika wanajihusisha na shughuli za maendeleo lakini bado kuna changamoto ya usawa wa kijinsia, jambo la kijisnia linagusa kila sehemu kuanzia serikalini, taasisi za kijamii, mashirika binafsi na hata kwenye vyombo vya habari,

"Kwa sasa Afrika ndiyo ya mwisho kwa maendeleo ya binadamu kulinganisha na sehemu zingine duniani na jambo la usawa wa kijinsia linabaki kuwa muhimu, UNDP itaendelea kushirikiana na serikali kusaidia kupatikana usawa wa kijinsia na uwezeshaji kwa wanawake ili kumaliza vitendo hivi ambavyo vinachangia Afrika kuwa nyuma kimaendeleo," alisema Dabo.


 Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Sihaba Nkinga akikata utepe kuashirikia kuzinduliwa kwa Ripoti ya Maendeleo ya Afrika 2016.
  Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Sihaba Nkinga akiwa na Mkurugenzi Mtendaji Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii (ESRF), Dk. Tausi Kida (wa  kwanza kushoto), Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Awa Dabo (wa tatu kulia), Mkuu wa Kitengo cha Jinsia kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Timothy Mgonja na Mwakilishi wa UN Women wakionyesha kitabu cha Ripoti ya Maendeleo ya Afrika 2016.
 Wageni rasmi wakiwa katika picha ya pamoja baada ya halfa ya uzinduzi wa Ripoti ya Maendeleo ya Afrika 2016.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...