Mkurugenzi Mkuu, Mh. James Kilaba
Na Mwandishi Maalum, Hammamet, Tunisia.

PAMOJA na maendeleo na faida mbalimbali za Tekinolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA), masuala ya Usalama, faragha na imani katika matumizi bado yameendelea kuwa masuala ya kuwekwa maanani katika ngazi za kitaifa na kimataifa.

Akihutubia kikao cha Mkutano wa Dunia wa Masuala ya Viwango Katika Mawasiliano (World Telecommunication Standardization Assembly – WTSA-16) mjini Jasmine Hammamet, nchini Tunisia hivi karibuni, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Eng. James Kilaba amesema tekinolojia mpya ndani ya TEHAMA zina mchango mkubwa katika usalama (wa mitandao,mifumo, vifaa, data na wa watumiaji); faragha ( katika data na watumiaji) na Imani (kwenye mitandao,mifumo, vifaa, data na kwa watumiaji). 

“Katika vikao kama hivi vya majadiliano kuhusu TEHAMA, wakati mwingi hatusahau kuzungumzia masuala ya huduma, vifaa na ukuaji wa watumiaji, mtandao na hata mapato. Leo tunazungumzia mchango wa teknolojia mpya katika usalama, faragha na Imani katika matumizi ya TEHAMA”, Mkurugenzi Mkuu wa TCRA aliuambia mkutano huo.

Eng. Kilaba ailisema kumekuwepo na mabadiliko ya teknolojia kutoka zilizotawaliwa kwa kiasi kikubwa na kuendeshwa kwenye mfumo wa intaneti kwa kutumia kompyuta binafsi zilizounganishwa kwa mfumo wa waya hadi tekinolojia zinazotumia vifaa ya mkononi vilivyounganishwa bila kutumia waya. Amesema hii imewezesha na kufanikisha mawasiliano zaidi na kwa kupitia mfumo wa intaneti kuifikia dunia iliyounganishwa na mfumo wa kompyuta.

Eng Kilaba aliongeza kwamba mada kuu ya majadioiano katika mkutano huo ilikuwa ni huduma, vifaa, kukua na kuongezeka kwa watumiaji na kupanuka na kwa mifumo ya mawasiliano ambayo inawafika mbali zaidi na kuwafikia watu wengi zaidi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...