Baadhi ya wafanyakazi wa Vodacom Tanzania,wakiongozana kutoa msaada wa nguo na vyakula mbalimbali kwa wodi ya watoto Njiti kwenye hospitali kuu ya Mnazi Mmoja Zanzibar jana kuelekea matembezi ya kesho kuadhimisha siku ya mtoto njiti duniani yatakayofanyika mjini Zanzibar.
 Muuguzi Mkuu wa hospitali ya Mnazi Mmoja Zanzibar, Magreth Sylvester(kushoto)akipokea baadhi ya vyakula mbalimbali  na nguo kwa ajili ya wodi ya watoto njiti hospitalini hapo jana toka kwa Mkuu wa Vodacom Tanzania kanda ya Zanzibar, Mansour Mansour(kulia)wapili kushoto ni Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa kampuni hiyo,Jacquiline Materu na Mwanzilishi wa Mfuko wa kusaidia watoto njiti,Doris Mollel.
 Muuguzi dhamana wa wodi ya watoto njiti katika hospitali kuu ya Mnazi Mmoja Zanzibar,Khadija Mgeni(kushoto)akitoa maelezo kwa Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom Tanzania,Jacquiline Materu na Mwanzilishi wa Mfuko wa kusaidia watoto njiti,Doris Mollel ,walipotembelea hospitali hiyo kutoa misaada ya vyakula mbalimbali na nguo jana katika hospitali hiyo. 
aadhi ya wahudumu wa wodi ya watoto njiti wa hospitali Kuu ya Mnazi Mmoja pamoja na wafanyakazi wa Vodacom Tanzania na Dorris Mollel Foundation wakiwa wamewabeba baadhi ya watoto hao waliopo katika wodi hiyo,wakati walitembelea hospitalini hapo kutoa misaada mbalimbali ya vyakula na nguo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...