SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Nchini (TFF) kupitia Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi (Kamati ya Saa 72) umeendelea kuwaweka kiporo waamuzi wa mchezo baina ya Yanga na Simba uliochezwa Oktoba 01 mwaka huu ambao ulichezeshwa na mwamuzi Martin Saanya pamoja na mwamuzi msaidizi namba moja Samuel Mpenzu.


Mwamuzi wa mchezo wa Mbeya City dhidi ya Yanga Rajab Mrope, Thomas Mkombozi aliyechezesha mechi ya Coastal Union Vs KMC nao uchunguzi wao unaendelea kukamilika huku hatua ya mwisho ya uchunguzi huo ni wao kufika mbele ya Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi (Kamati ya Saa 72) ambapo watahojiwa ili kutoa ufafanuzi katika masuala mbalimbali yaliyojitokeza katika taarifa zao.


Katika mchezo wa Yanga na Simba, Saanya alishindwa kuhimili mchezo huo na kupelekea mashabiki wa klabu ya Simba kufanya vurugu baada ya kukubali goli lililofungwa na Mrundi Amisi Tambwe na kisha wachezaji wa timu ya Simba kumzonga na kumpa kadi nyekundu Jonas Mkude ambayo baadae kamati ya masaa 72 iliweza kuifuta na kumruhusu kuendelea kucheza mechi za ligi kuu.

Mpenzu ambaye alikuwa mwamuzi msaidizi wa mchezo huo, alionyesha udhaifu kwa kukataa goli halali la Ibrahim Ajib kuwa kuonyesha kuwa ameotea.

Katika mechi ya Mbeya City dhidi ya Yanga uliopigwa kwenye uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya, mwamuzi Rajab Mrope naye amepewa muda wa kujieleza mbele ya kamati ya masaa 72 baada ya kuonyesha madhaifu kwenye mchezo huo kwa kutoa maamuzi tofauti mara tatu baada ya goli la pili lililofungwa na timu ya Mbeya City kuwa na utata na timu ya Yanga kulalamika.

Naye Kamishna wa mechi ya Tanzania Prisons na Simba Jimmy Lengwe kutoka Morogoro amepewa onyo kali kwa kutoripoti baadhi ya matukio ya wazi yaliyotokea kabla ya mechi hiyo kuanza.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...