WALIMU wastaafu nchini wameanzisha jukwaa maalum litakalotumika kwa ajili ya kushauriana na kubadiliana uzoefu baina yao na serikali kuhusu mfumo na utaratibu utoaji bora wa elimu nchini.
Hayo yamesemwa leo, Jijini Dar es Salaam na mwenyekiti wa jukwaa hilo Prof. Herme Mosha alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari juu ya lengo la uanzishwaji wa jukwaa hilo.
Prof. Mosha alisema walimu wastaafu wana uzoefu mkubwa katika sekta ya elimu hivyo kupitia jukwaa hilo watakuwa wakitafakari maeneo ambayo sekta ya elimu  haitoweza kufanya vizuri na hivyo kuishauri hatua zinazopaswa kuchuliwa na Serikali.
“Unapokuwa mtumishi wa Umma unaona kila kitu kinaenda sawa, lakini unapokuwa nje unaona kuna mambo mengi ambayo yalikuwa hayaendi sawasawa,” alifafanua Prof. Mosha.
 Mwenyekiti wa Jukwaa la  Wastaafu wa Taaluma ya Elimu, Profesa Herme Joseph Mosha akizungumza na waandishi wa habari kuhusu wakati wa kukitambulisha rasmi Jukwaa hilo katika Ukumbi wa Idara ya Habari –MAELEZO leo jijini Dar es Salaam. Kutoka kushoto ni wajumbe wa Sekretarieti ya chama hicho Bibi. Khadija Mchatta Maggid na Muhwela Kalinga.
 Katibu Mtendaji wa Jukwaa la Wastaafu wa Taaluma ya Elimu, Bibi. Marystella Maufi Wassena akifafanua jambo wakati wa mkutano wa kukitambulisha Jukwaa hilo leo jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mwenyekiti wa Jukwaa hilo Profesa. Herme Joseph Mosha

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...