Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS), Dk. Leonard Maboko akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam juzi, ambapo aliwaasa wananchi kuchukua uamuzi wa  kupima afya zao na kupatiwa matibatu. Kulia ni Mwenyekiti wa Tume hiyo, Dk. Hedwiga Swai. 

Na Dotto Mwaibale
WANANCHI wametakiwa kupima kila wakati na kuendelea kutumia kinga ili kujiepusha na maambuki mapya ya VVU.
Mwito huo umetolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS), Dk. Leonard Maboko katika kikao cha makamishina wapya wa tume hiyo kilichoketi jijini Dar es Salaam juzi. 
"Tunapaswa kuwa ni mikakati endelevu ya kupambana na ugonjwa wa ukimwi kwani bado kunachangamoto kubwa" alisema Maboko.
Maboko alisema watanzania wasidanganyike kuwa ukimwi umekwisha ugonjwa huo bado upo na ni changamoto kubwa.
Alisema changamoto kubwa ya ugonjwa huo bado ipo katika baadhi ya mikoa hasa ile ya nyanda za juu kama Iringa na Njombe hivyo wananchi wasibweteke kuwa ugonjwa huo umekwisha.
Alisema kwa Tanzania Bara kunamaambukizi ya asilimia 5.3 sawa na watu milioni mbili waliopata maambukizi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...