Mwenyekiti wa Mfuko wa Wanawake Tanzania, Profesa Ruth Meena (katikati) akisoma tamko la wanawake kwa wanahabari kuelezea tathini ya mwaka mmoja wa Serikali ya awamu ya tano mara baada ya kufunguliwa kwa mkutano huo. Wengine ni viongozi na wajumbe wa mkutano huo.

WANAWAKE kupitia Mfuko wa Wanawake Tanzania wamekutaka katika mkutano na kutoa tathimini ya mwaka mmoja wa Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dk. John Pombe Magufuli. Mkutano huo ulioshirikisha wanawake kutoka mikoa mbalimbali umefanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Mtandao wa Jinsia Tanzania, TGNP Mabibo jijini Dar es Salaam.

Akizungumza katika mkutano huo, Mwenyekiti wa mfuko huo, Profesa Ruth Meena aliipongeza Serikali ya Dk. Magufuli kwa mafanikio ilioanza kuonesha katika ukusanyaji na usimamizi wa mapato pamoja na mapambano dhidi ya vitendo vya rushwa huku akiiomba Serikali kutambua pia kwa vitendo mchango wa wanawake katika ujenzi na maendeleo ya nchini. Aliyekuwa mgombea nafasi ya urais wa Chama cha ACT – Wazalendo, Anna Mghwira (kulia) ambye pia ni Mwenyekiti wa chama hicho taifa akichangia mada katika mkutano wa wanawake ulioandaliwa na Mfuko wa Wanawake Tanzania. Baadhi ya washiriki katika mkutano huo wakijadiliana masuala anuai. Mkutano huo ulioshirikisha wanawake kutoka mikoa mbalimbali umefanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Mtandao wa Jinsia Tanzania, TGNP Mabibo jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa WFT, Mary Rusimbi (kushoto) akichangia mada katika mkutano huo.
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...