Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii 

WASOMI wanazuoni wametakiwa kutumia maarifa walionayo kwa lengo la kusaidia kukua kwa elimu na Uchumi katika umoja wa jumuiya ya Afrika Mashariki .

Hayo yamesemwa na Balozi Ramadhani mwinyi, alipokuwa akisoma hotuba kwa niaba ya Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki, Augustine Mahiga katika ufunguzi wa mkutano wa vyuo vikuu vya Serikali na watu binafsi.

“kama jumuiya lazima tuhakikishe kuwa tunatoa elimu kwa wanataaluma ambayo itawasaidia kuwakwamua kiuchumi kwa kuzalisha wasomi ambao wataweza kutoa ajira kwa wengine na sio wale watakao tegemea ajira kutoka kwa wengine”amesema Mwinyi.

Amesema kuwa elimu inayopatikana kutokana na tafiti mbalimbali zinazofanywa inatakiwa zisadie katika ukuaji wa maendeleo katika ukanda wa Afrika Mashariki.
  Katibu  mkuu wa Baraza la vyuo vikuu Afrika Mashariki , Profesa Alexandre  Lyambabaje.
 Balozi Ramadahani Mwinyi amabye alimwakilisha waziri wa mambo ya neje na ushirikiano Afrika Mashariki 
 baadhi ya washiriki katika kongamano hilo wakifatilia kwa makini.
Mtoa mada wa kwanza  Liliani Awenja akizungumza wakati wa kongamano hilo lilifanyika katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere Dar es Salaam
 Joseph Njogu kutoka  ResearchAfrica akitoa maelezo kwa Balozi Ramadhani Mwinyi alipokuwa akitembelea maonyesho.
 wajumbe kutoka Stramore Univesity ya Nairobi kenya wakiwa katika picha ya Pamoja na mgeni rasmi.
Balozi Ramadhani Mwinyi akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mkutano huo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...