Judith Mhina - Maelezo

Wazazi Halmashauri ya Kakonko, wafanikiwa kutoa chakula katika shule 59 zilizopo katika Halmashauri hiyo kuamzoa mwaka  2015.

Mkoa wa Kigoma una jumla ya Halmashauri 8 na kati ya hizo ni Kakonko peke yake ndio imefanikiwa kutoa huduma ya uji shuleni. Nikiongea na Waratibu kata kata 5 za Kakonko Bw Jobson Johnston, Scolastica Andrew, Paschal Mlelema, Eliud Kayigwe na Samson Sike kwa wakati mmoja wamesema hatukujua kama Halmashauri nyingine hawana huduma hiyo katika shule zao walidhani ni mpango wa Mkoa 

Hata hivyo, walisema:” Changamoto walizoziainisha waratibu Kata wa Halmashauri nyingine hazina mashiko hivyo ni vema wakajithatiti kuhamasisha  wazazi nina hakika wakielewa umuhimu wa chakula shuleni , watakubali kuchangia na hatimaye watoto watapata Uji na kutoa huduma hiyo.
Watoto wa Shule ya Msingi ButaLe Maalum wakipata Chakula cha Mchana shuleni

Waliongeza kwa kusema utafiti wa Shirika la Kimataifa la Watoto UNICEF uliofanyika 2001-2003,  ulionyesha watoto waliowengi wa shule za msingi Mkoa wa Kigoma wamedumaa kwa kubeba mizigo mikubwa kuliko uwezo wao na kukosa chakula bora, wakati Mkoa unakila aina ya chakula, na kuongeza mafuta ya mawese matunda mbogamboga za majani yote yanayopatikana Tanzania yapo Kigoma, , hivyo  hakuna sababu ya msingi ya watoto kudumaa. 

Mratibu Kata kiongozi wa Kakonko kwenye Warsha ya Mpango wa Kuinua Kiwango cha Elimu, Bw Jobson Johnston alisema kila mzazi anachangia kilo 5 ya mahindi, hivyo shule kupata mahindi zaidi ya mahitaji ya mwaka , ambapo huuza kiasi kwa ajili ya  kupata fedha ya kununulia maziwa, sukari na mafuta ya mawese. 

Uji unaotolewa mashuleni umekuwa na virutubisho bora kabisa kumfanya mwanafunzi apate usikivu wamasomo darasani, nakuweza kufanya vizuri.Kila mwanafunzi huja shule na kikombe chake kwa ajili ya huduma ya kupata uji. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...