Na Nathaniel Limu- Singida.
Waziri wa mambo ya ndani Mhe. Mwigulu Lameck Nchemba (mb), ameliagiza jeshi la polisi nchini,kuwakamata na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria madereva wanaoacha mawe na matawi ya miti barabarani.
Nchemba ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Iramba mkoani Singida, ametoa agizo hilo wakati akizungumza kwenye kikao cha 38 cha bodi ya barabara mkoa kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa ofisi ya mkuu wa mkoa mjini hapa.
Amesema baadhi ya madereva wa magari na hasa yale makubwa,hutumia mawe kuzuia magari yao kutembea wakati wakiyafanyia matengenezo ya dharura.
“Wakiisha maliza kuyafanyia matengenezo magari yao, madereva hao huyaacha barabarani mawe na matawi ya miti ambayo hutumika kutoa tahadhari kwa vyombo vingine vya moto. Kitendo hicho kinahatarisha maisha na mali za watumiaji wengine wa barabara kwa vile yanaweza kusababisha ajali”, amesema Mwigulu.
Waziri wa Mambo ya ndani Mhe. Mwigulu Lameck Nchemba akiwa katika kikao cha 38 cha bodi ya barabara ya Mkoa wa Singida.
Mkuu wa Mkoa wa Singida na Mwenyekiti wa Bodi ya barabara Mkoani hapa Mhandisi Mathew John Mtibumwe akiendesha kikao cha 38 cha bodi ya barabara ya Mkoani hapa, Kulia kwake ni Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Singida Mhe, Martha Mlata.
Meneja wa TANROADS Mkoani Singida Mhandisi Leonard Kapongo akijibu baadhi ya hoja katika kikao cha 38 cha bodi ya barabara ya Mkoa wa Singida.
Wajumbe na wadau mbalimbali wa bodi ya barabara wakichangia hoja katika kikao cha 38 cha bodi ya barabara ya Mkoa wa Singida.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...