Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb) (katikati), akipeana mkono na Balozi wa Finland nchini Tanzania Pekka Hukka (kulia),  baada ya kumalizika kwa Mkutano kati ya Tanzania na Finland kuhusu Ushirikiano wa Maendeleo katika Sekta ya Nishati, Biashara, Kilimo na Mawasiliano. Kushoto ni Waziri wa Mambo ya Nje, Biashara na Maendeleo wa Finland Kai Mykkanen, Mkutano huo umefanyika katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango, jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb) (kulia), akifafanua jambo kwa wajumbe kutoka Serikali ya Finland (hawapo pichani), Kushoto ni Kamishna Msaidizi wa Ushirikiano wa Kikanda kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Judica Omary.
 Waziri wa Mambo ya Nje, Biashara na Maendeleo wa Finland, Kai Mykkanen (kulia), akizungumza katika Mkutano kuhusu Ushirikiano wa Maendeleo katika Sekta mbalimbali ikiwemo  Kilimo, Biashara, Mawasiliano na Nishati, kati ya Tanzania na Finland . Kushoto ni Balozi wa Finland nchini Tanzania Pekka Hukka, Mkutano huo umefanyika katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.

 Wajumbe kutoka Serikali ya Finland (kushoto) na wenyeji wao kutoka Tanzania (kulia) wakiwa katika mkutano wa pamoja wakijadili kuhusu masuala ya Ushirikiano wa Maendeleo katika Sekta mbalimbali ikiwemo Kilimo na Nishati, kati ya pande hizo mbili, Mkutano huo uliofanyika katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango, Jijini Dar es Salaam.
Picha zote na Kitengo cha Mawasiliano, Wizara ya Fedha na Mipango

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...