Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini (RITA) kwa kushirikiana na wadau mbalimbali imebuni na kuanza kutekeleza mpango wa Usajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa bure kwa watoto wenye umri chini ya Miaka mitano.
Akizungumza na wanahabari Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu RITA Emmy Hudson amesema kuwa mpango huo umebuniwa ili kuleta suluhisho la changamoto iliyokuwa ikisababisha watoto kushindwa kusajiliwa na kupata vyeti vya kuzaliwa kwa wakati.
Aidha amesema kuwa mpango huo ambao ulianza katika Mikoa ya Mwanza, Mbeya na Songwe hivi karibuni ulizinduliwa katika mikoa ya Iringa na Njombe hivyo basi ni mpango endelevu na wa kudumu.
Emmy ameongeza kuwa utekelezaji huo umefanikiwa kwa mikoa hiyo ambapo Njombe imepanda kutoka 8.5% ya watoto walisajiliwa hadi kufikia 98%.
Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini (RITA) Emmy Hudson akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya Usajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa bure kwa watoto wenye umri chini ya Miaka mitano leo jijini Dar es Salaam.kuliani Meneja Usajili (RITA) Angela Anatory na kushoto ni Mkurugenzi wa Tehama(RITA) Cuthbert Simalenga
Meneja Usajili (RITA) Angela Anatory akifafanua jambo katika mkutano uliofanyika leo jijini Dar es Salaam lishoto ni Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini (RITA) Emmy Hudson
Sehemu ya waandi wa habari wakimsikiliza Kaimu Afisa Mkuu wa Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini (RITA) Emmy Hudson.picha na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...