Judith Mhina - MAELEZO.

Nidhamu katika Utumishi wa Umma inayosisistizwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli Imeiweka Tanzania katika ramani ya dunia.
Hayo yamesemwa na Balozi Christopher Liundi katika mahojiano kwa njia ya simu yaliyofanyika jana jumapili. Mheshimiwa Balozi Liundi alisema;
Tanzania sasa dunia nzima, na ndivyo ilivyokuwa kwa Tanzania utakumbuka enzi za Baba wa Taifa. Rais wetu anaifufua ile ari na  kurejesha heshima iliyokuwepo hapo awali ;Ameeleza kwamba nidhamu katika kila kitu ni jambo la msingi sana, iwe katika utumishi wa Umma au wa Sekta binafsi, barabarani, Nidhamu inatakiwa itoke moyoni mwako na ufurahie hali ya kuwa na nidhamu. Nidhamu katika Utumishi wa Umma ni lazima ni msingi kwa vijana wetu katika kupata ajira bila ya malamiko kutokana na Waajiri na wadau wengine kuwa vijana hawafanyi kazi au wavivu, hawana nidhamu, na viwango.
Balozi Liundi amefafanua kuwa, enzi za Baba wa Taifa unapokwenda popote duniani, ukisema niketoka Tanzania kila mtu anajua Mtanzania ni mkweli, muwazi  na ana nidhamu ya hali ya juu. Mtanzania hawezi kupokea wala kutoa rushwa, hashiriki kwenye masuala yoyote ya kuiharibia heshima nchi yake, mwenye kutumia madaraka yake vizuri, na asiyefuja mali ya umma.Amesema wakati umefika kwa Watanzania kumuunga mkono Rais wetu katika kuhakikisha kwamba nidhamu katika utumishi wa Umma inakuwepo.
Akiongea kuhusu miaka 55 ya Uhuru wa Tanganyika Balozi Liundi amesema kauli ya Rais Magufuli la kutaka Taifa liondokane na umasikinini kwa kufufua au kujenga viwanda vidogo vya kati na vikubwani lazima utekelezwe.
Balozi Liundi amempongeza Rais kwa jitihada zake za kuwaweka katika utayari wafanyabiashara binafsi wa Tanzania katika kujenga viwanda. Akiongea na wananchi alipokwenda kufungua kiwanda cha matunda cha Azam cha Salim Said Bahkresa atahakikisha changamoto zilizopo kama umeme kwa kuagiza TANESCO wamfungie umeme na kumpa shamba la hekari 1000 bure ili kupanda miwa kwa ajili ya kuzalisha sukari. “Kazi ya Serikali ni kuweka mazingira mazuri ya uwekezaji ambao kwa vitendo Rais amelithibitisha hili”.
Pia nampongeza kwa kuanzisha mfumo unaomtaka kila mfanyabiashara kuwa na mashine za kulipa kodi: “Mpaka sasa imefikia mahali nchi nyingine za nje wameanza kuiga utendaji wa kazi wa Rais wetu hili ni jambo la kujivunia”. Hivyo tumuunge mkono katika hii vita ya ukusanyaji kodi. 
Tunapoadhimisha miaka 55 ya Uhuru wetu tukumbuke kauli ya Mwalimu Nyerere alisema: “ UHURU  NA KAZI”, ni kweli kabisa lazima tufanye kazi kama anavyosisitiza Rais wetu  Magufuli “HAPA KAZI TU”. Maendeleo hayaji kwa kupiga hadithi ni lazima watu wafanye kazi na asiyefanya kazi na asile.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...