Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Viongozi wakati alipowasili katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Tunguu (Zanzibar University) Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja akiwa mgeni rasmi katika Mahfali ya Kumi na Nnne yaliyofanyika Chuoni hapo.
Mkuu wa Chuo Kikuu cha Zanzibar Tunguu,pia Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini Prof.Suleiman Bin- Nassry Basahal alipokuwa akiwatunuku Stashahad na Shada wahitimu katika fani mbali mbali wa mwaka 2016 wakati wa sherehe ya Mahfali ya kumi na nne yaliyofanyika leo katika Chuo hicho huko Tunguu Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akipokea zawadi kutoka wa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Zanzibar Tunguu,pia Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini Prof.Suleiman Bin- Nassry Basahal wakati wa sherehe ya Mahfali ya kumi na nne iliyofanyika leo katika Chuo hicho huko Tunguu Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akitoa hutuba yake wakati wa sherehe ya mahfali ya kumi na nne (14) katika Chuo Kikuu cha Tunguu (Zanzibar University) Wilaya ya Kati,Mkoa wa Kusini Unguja,(kulia) Prof.Saleh Idriss Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo na (kushoto) Mkuu wa Chuo Kikuu cha Zanzibar Tunguu,pia Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini Prof.Suleiman Bin- Nassry Basahal.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...