Na Amina Kibwana,Globu ya Jamii

Kampuni ya Uwekezaji ya Taifa (NICOL) inatarajia kurudi upya mara baada ya kuingia hasara ya sh. Billion 10 pamoja na kukabiliana na kesi Mbalimbali ikiwemo  kupinga maamuzi ya wanahisa kuchagua uongozi pamoja na maamuzi ya kusitishwa kwa mkutano mkuu uliolenga kuzungumzia maswala ya mahesabu na muelekeo wa Kampuni.

Akizungumza na waandishi wa Habari  Mwenyekiti wa NICOL Dk. Gideon Kaunda amesema kuwa kesi ya mwisho ya 41 iliamuliwa  mahakamani mara baada ya Mlalamika  makamu mwenyekiti wa TPSF Salum Shamte kutokuhudhuria mahakamani na hoja hizo zilikataliwa na Mahakama kuamua kuwa mkutano huo ulikuwa wa halali na ambapo mnamo Novemba 26 mkutano huo uliendelea.

“Mkutano ulikwenda vizuri ambapo zaidi ya watu 300 kutoka mikoa mbalimbali walihudhuria pamoja na mashirika mbalimbali ya umma ambayo yalikuwa yamewekeza  wakiwemo PSPF, walifanikiwa kuhudhuria”. Alisema Kaunda 

Aidha alisema kuwa Kampuni hiyo iliingia hasara kutokana na  uongozi uliopita kuwa na malimbikizo ya sh. Billion 10 kutokana na mahesabu yaliyofanywa, ambayo taarifa ilionesha kuwa kampuni ilikuwa inapata faida kwa wakati huo  sio sahihi,pamoja na kutokufuatwa kwa sheria na utovu wa nidhamu.

Kwa upande wake Mtendaji  Mkuu wa NICOL  Adam Wanuza amesema kuwa kuwa pamoja na hasara hiyo,ukiwemo uwekezaji mbovu umechangia kutokana na makampuni mbalimbali kuchukua mkopo katika Kampuni ya Nicol.

Naye Naibu Waziri Mstaafu katika sekta ya Uchukuzi ambaye pia ni Mtaalamu katika Masuala ya Biashara Dk. Athumani Mfutakamba amesema kuwa kufanikiwa kwa Mkutano huu ni ishara tosha ya kuzaliwa upya kwa NICOL katika jitihada za Kampuni ya uwekezaji ya kizalendo na jitihada hizi lazima ziungwe mkono na wazalendo wote wanaotaka maendeleo ya uchumi wa Taifa la Tanzania katika fursa mbalimbali.

Kampuni ya Nicol itarudi Rasmi kupitia uongozi mpya sambamba na kuanza kutoa elimu Maalumu kwa wawekezaji katika soko la Hisa mnamo mwanzoni mwa mwaka 2017.
Mwenyekiti wa kampuni ya Uwekezaji wa Taifa (NICOl) Bw. Gideon Kaunda kulia akisisitiza jambo mbele ya waandishi wa habari hawapo pichani wakati wa mkutano na waandishi wa habari uliofanyika jijini Dar es salaam mara baada ya kupata uongozi mpya wa kampuni hiyo ulioteuliwa rasmi hivi karibuni na bodi ya NICOL kushoto ni Mtendaji Mkuu Bw. Adam Wamunza.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...