Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

LIGI kuu Tanzania Bara inatarajiwa kuendelea tena kwa duru la pili kuanzia Desemnba 17, huku timu zikishauriwa kukamilisha usajili kwa wakati huku Yanga na Simba kuumana Februari 18 2017..

Dirisha la usajili lililofunguliwa Novemba 15 linatarajiwa kufungwa Desemba 15 na timu zote zimeopewa mwongozo wa kutumia mfumo wa ule ule wa kutumia mtandao katika kuwasilisha majina hayo usiku wa Desemba 15.

Ofisa habari wa Shirikisho la Mpira wa Miguu (TFF) Alfred Lucas amesema kuwa ligi inatarajiwa kuanza Desemba 17 kwa mechi nne kuchezwa kwenye viwanja tofauti nchini.

Lucas amesema kuwa kwa sasa ratiba hii imezingatia kalenda ya michezo ya kimataifa, kombe la mapinduzi na kombe la Shirikisho ilihali hawajaweza kuweka ratiba ya michezo ya kimataifa kwa timu zinazoshiriki michuano hiyo kwani ratiba ya Shirikisho la Mpira Afrika bado hawajaweka raiba wazi.

Katika ratiba hiyo, Kikosi cha Simba kitaanzia ugenini kuvaana Ndanda huku mabingwa watetezi Yanga wakiwa Uwanja wa Taifa kuumana na JKT Ruvu na Azam watakuwa ugeninio dhidi ya African Lyon.

Ofisa habari wa Shirikisho la Mpira wa Miguu (TFF) Alfred Lucas

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...