Na Woinde Shizza, Globu ya Jamii - Arusha 

BARAZA la madiwani Halmashauri ya Meru mkoani Arusha wamkaanga Mkurugenzi wao kwa kusema hana uwezo wa kuongoza Halmashauri hiyo.


Akitoa maazimio ya kikao cha baraza kilichokaa siku mbili kwa kuwajumuisha madiwani, wakuu wa idara mbalimbali na wataalam, Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Willy Njau Alisema wametafakari kwa kina utendaji wa Mkurugenzi na kubaini kuwa hafai. "Tumejadili ajenda ya utendaji usioridhisha wa Mkurugenzi wetu na tumeona kuwa haufai kutokana na mambo mengi anayoyafanya yanakiuka kanuni na taratibu za Halmashauri"alisema Njau.

Aidha Njau alisema Mkurugenzi huyo ameonekana kukata mawasiliano na Mwenyekiti wa Halmashauri jambo alilosema siyo sahihi. pia ameweza kukata mawasiliano na madiwani wa Halmashauri hiyo pamoja na kusababisha hata wakuu wa idara kutokuwa na mawasiliano na madiwani jambo linalorudisha maendeleo nyuma.
Aliongeza kuwa Mkurugenzi huyo ameshindwa kukusanya makusanyo ya pesa kiasi cha milioni 150 kilichokusudiwa kukusanywa tangu Julai hadi Septemba mwaka huu jambo alilosema linaweza kusababisha Halmashauri kutopewa ruzuku kutoka serikalini kwasababu ya uzembe.


" Tumejiridhisha kuwa uwezo wa Mkurugenzi kuiongoza Halmashauri yetu kama Mkurugenzi Mtendaji ni mdogo hivyo hafai anadidimiza maendeleo ya Halmashauri ya meru" alisema Njau. Na kuongeza "Tumeamua kuiomba mamlaka yake na Uteuzi ichukue hatua stahiki za kumuwajibisha ili kunusuru maendeleo ya Halmashauri ya Meru".



Vilevile alisema kuwa Mkurugenzi huyo amekuwa akidharau maagizo yanayotolewa na kamati mbalimbali za baraza hilo na Kushindwa kuzitekeleza, ambako ni kuvunja kanuni na taratibu za Halmashauri. Hata hivyo alisema kitendo cha Mkurugenzi kukata posho za madiwani ni kinyume na utaratibu kwani ziliwekwa kisheria ambapo alisema Kama kuna tatizo la kukatwa posho ni lazima sheria hiyo ingebadilishwa kwanza. "Mwenye dhamana ya kutangaza kuwa posho zinabadilika ni Waziri mwenye dhamana hiyo lakini siyo Mkuu wa Mkoa, Wilaya au Mkurugenzi" alisema.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Meru, Christopher Kazer akijibu hoja za Madiwani katika kikao cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri hiyo.


Naye Diwani wa Kikatiti Elisa Mungure ambaye ni Mwenyekiti wa madiwani alisema Mkurugenzi huyo amekuwa akiendesha Halmashauri kisiasa jambo ambalo halifai. "Ninasikitishwa na uongo unaoelezwa na Mkurugenzi ambaye kateuliwa na Mheshimiwa Rais hii ni ajabu haiwezekani kuendelea kumuamini mtu wa aina hii" alisema Mungure.

BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...