Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb) akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Jengo la pili la Taaluma lenye ghorofa 7 la Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini Kampasi Kuu ya Dodoma, lililogharimu shilingi Bilioni  10.3. Kulia kwake ni Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi wa Chuo hicho Prof. Razack Lokina na kushoto kwake ni Mkuu wa Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini Dkt. Frank Hawassi wakifurahi kwa pamoja mara baada ya uzinduzi huo.
  Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango, akiangalia viatu vya ngozi vilivyotengenezwa na mjasiliamali mdogo Bw. Stephano Chifwaguzi (nayeonesha bidhaa ya ngozi kiunoni) baada ya kuwezeshwa kiutaalamu na Chuo cha Mipango na Maendeleo Vijijini, kwa ufadhili wa Jumuiya ya Ulaya, wakati wa mahafali ya 30 ya Chuo hicho Kampasi Kuu ya Dodoma.
 Meza Kuu ikiongozwa na Mgeni Rasmi, Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb) akifurahia mahafali ya 30 ya Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini, yaliyofanyika Kampasi Kuu ya Dodoma katika eneo la Miyuji-mkoani humo.
 Wajumbe wa Baraza la kumi na la tisa la uongozi wa  Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini wakiimba wimbo wa Taifa wakati wa Mahafali ya 30 ya Chuo cha Mipango na Maendeleo Vijijini Kampasi ya Dodoma, iliyoko katika eneo la Miyuji, mkoani humo.
Wahitimu wa Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini pamoja na wageni waalikwa, wakiimba wimbo wa Taifa wakati wa Mahafali ya 30 ya Chuo hicho yaliyofanyika katika eneo la Miyuji, mkoani Dodoma.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...