Na Zainab Nyamka,
Globu ya Jamii
Globu ya Jamii
MAHAFALI ya 10 Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) yafana kwa wahitimu 944 kutunukiwa shahada mbalimbali za masomo ya Afya huku Mkuu wa Chuo Rais Mstaafu, Alhaji D Ali Hassan Mwinyi akiwatunukiwa wanafunzi saba shahadan ya uzamivu.
Mahafali hayo yaliyofanyika leo Jijini Dar es salaam, Makamu Mkuu wa Chuo MUHAS, Ephata Kaaya amesema kuwa azma ya Chuo chao ni kuwa na wanafunzi wa kike na wakiume kwa idadi sawa kwani katika mwaka huu wa mahafali wanafunzi 372 sawa na aslimia 39.4 ni wanawake kwa hiyo bado wanaendela na mpango wa kuwawezesha wanafunzi wa kike kujikunga na programu mbalimbali zinazotolewa hapa chuoni.
Kaaya amesema kuwa , katika kuendeleza kutoa nafasi kwa wanafunzi MUHAS wamefanikiwa kupata imefanikiwa kukamilisha ukarabati wa kliniki mpya ya wagonjwa wa afya ya kinywa na meno watakaokuwa wanajilipia wenyewe na vifaa tiba vimeshapayikana kutoka shirika lisilo la kiserikali la The Miracle Corners Of the World (MCW)la Nchini Marekani na vinategemewa kuwaili nchini na kufungwa kwenye kliniki hiyo mwezi Januari.
Katika ,mahafali hayo, wahitimu saba waliweza kutunukiwa shahada za uzamivu kwa kufanya tafiti mbalimbali za magonjwa na dawa ambao ni Siana Nkya,Ramadhan Nondo, Dickson Mkoka, Gladys Mahiti, Grace Shayo, Coline Mahende na Richard Mwaiselo.
Mkuu wa Chuo pia aliweza kuwatunukiwa wahitimu wawili wa shahada ya uzamili wa Sayansi Maalumu ambao ni Mohamed Mnacho na John Ngendahayo huku wahitimu nane wakipatiwa shahada ya juu katika masuala mbalimbali pia 183 shahada ya uzamili na wahitimu 376 walitunukiwa stashahada,
Makamu Mkuu wa Chuo Cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) Profesa Ephata Kaaya akitoa hotuba kwa wahitimu wa Chuo hicho katika mahafali ya 10 yaliyofanyika leo Jijini Dar es salaam, Kulia ni Mkuu wa Chuo hicho cha MUHAS, Rais Mstaafu Alhaji Ali Hassan Mwinyi na Mwenyekiti wa MUHAS Mariam Joy Mwafisi.
Mkuu wa Chuo
Cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (
Mkuu wa Chuo Cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS), Rais Mstaafu Alhaji Ali Hassan Mwinyi akimtunuku Shahada ya uzamivu (PhD) Grace Shayo katika mahafali ya 10 yaliyofanyika leo Jijini Dar es salaam.
|
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...