Makamu wa
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amesema Serikali
ipo mbioni kupunguza muda wa utoaji wa leseni za biashara nchini ili kutoa
fursa kwa wananchi wengi zaidi kupata leseni hizo kwa ajili ya shughuli za
kibiashara.
Makamu wa
Rais Samia Suluhu Hassan ametoa kauli hiyo jijini Dar es Salaam katika ukumbi
wa mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere wakati anafungua mkutano wa
wadau wa kuendeleza maeneo tengefu ya viwanda vya usindikaji wa vyakula nchini.
Makamu wa
Rais amesema mpango utaenda pamoja na kupunguza baadhi ya kodi na tozo ambazo
ni kero kwa wananchi hasa wenye viwanda kama hatua ya kukuza biashara na
uwekezaji katika sekta ya viwanda nchini.
Amesisitiza
kuwa Serikali inaendelea na mazungumzo na wenye mabenki hususani benki ya TIB
ili kutoa mikopo yenye riba nafuu kwa wawekezaji wenye nia ya kuanzisha viwanda.
Kuhusu
usindikaji wa bidhaa nchini, Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan ambaye pia ni
Mjumbe katika jopo la Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa la kumuwezesha mwanamke
kiuchumi akiwakilisha nchi za ukanda wa Kusini na Mashariki mwa Afrika
amepongeza jitihada zinazofanywa na wasindikaji wadogo nchini katika
utengenezaji wa bidhaa mbalimbali ambazo zitakidhi katika masoko ya ndani na
nje ya nchi.
“Serikali inafarijika sana kuona kuwa wasindikaji wadogo nchini
wamethubutu na wana uwezo wa ushindani katika biashara ya ndani na hata nje,
hivyo tunayohaki ya kujigamba kwa kuthubutu, Tumeweza na Tuendelea Kusonga mbele”
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia
Suluhu Hassan amesema umefika wakati kwa Wizara na taasisi za Serikali na wadau
wa maendeleo kuona umuhimu wa kuhakikisha viwanda vinajengwa vijijini ili
mkulima mdogo anapolima awe na uhakika wa kupata soko katika viwanda hivyo.
Amesema kuwa hali hiyo itaondoa changamoto ya kusafirisha bidhaa
nyingi ambazo zinaharibika njiani au zinapofika sokoni na hivyo kukosesha jamii
kipato kilichotarajiwa.
Makamu wa Rais pia amehimiza watafiti nchini wajielekeza
katika kufanya tafiti ambazo zitasaidia sekta binafsi na serikali kwa ujumla kuhusu
namna bora ya kukuza sekta ya viwanda nchini.
Kwa upande wake, Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji
Charles Mwijage amekiri kuwa bado kuna changamoto kubwa ya maeneo ya
yatakayojengwa viwanda na kwamba Serikali
imeliona tatizo hilo na inalifanyia kazi ambapo tayari imeshaziagiza Halmashauri zote nchini kujenga
maeneo kwa ajili ya viwanda.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakati ufunguzi wa mkutano wa Wadau wa kuendeleza maeneo Tengefu ya Viwanda vya Usindikaji Vyakula uliofanyika kwenye ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakati ufunguzi wa mkutano wa Wadau wa kuendeleza maeneo Tengefu ya Viwanda vya Usindikaji Vyakula uliofanyika kwenye ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam ambapo aliwapongeza TAPOFA kwa kazi nzuri wanayoifanya lakini pia aliwataka Wasindikaji kuongeza ushirikiano ili kufikia maendeleo na mafanikio ya juu.
Wadau waliohudhuria na kushiriki wakimsikiliza kwa makini Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakati ufunguzi wa mkutano wa Wadau wa kuendeleza maeneo Tengefu ya Viwanda vya Usindikaji Vyakula uliofanyika kwenye ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa TAFOPA Bi. Suzy Laizer akihutubia wakati ufunguzi wa mkutano wa Wadau wa kuendeleza maeneo Tengefu ya Viwanda vya Usindikaji Vyakula uliofanyika kwenye ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam, mgeni rasmi kwenye mkutano huu alikuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiangalia bidhaa mbalimbali za vyakula vilivyosindikwa zinazotengenezwa na wajasiriamali muda mfupi kabla ya kufungua wa mkutano wa Wadau wa kuendeleza maeneo Tengefu ya Viwanda vya Usindikaji Vyakula uliofanyika kwenye ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...