Wanafunzi wa shule mbalimbali za sekondari za jijini Dar es Salaam, wakimsikiliza kwa makini Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya usafiri wa Anga Tanzania(TCAA) Vallery Chamulungu wakati akiongea na kuzindua Kongamano la siku moja la maadhimisho ya siku Usafiri wa anga Duniani(ICAD) yaliyofanyika makao makuu ya (TCAA) Ukonga Banana jijini Dar es Salaam. Lengo kuu la kongamano hilo ilikuwa ni kuwahamasisha wanafunzi hao wapende masomo yanayohusiana na usafiri wa Anga.
Afisa mwanadamizi Idara ya uongozaji ndege Mwanajumaa Kombo akitoa elimu juu ya masuala ya uongozaji wa ndege kwa wanafunzi wa shule mbalimbali za sekondari za jijini Dar es Salaam, wakati wa Kongamano la siku moja la maadhimisho ya siku Usafiri wa anga Duniani(ICAD), yaliyofanyika makao makuu ya (TCAA) Ukonga Banana jijini Dar es Salaam. Lengo kuu la kongamano hilo ilikuwa ni kuwahamasisha wanafunzi hao wapende masomo yanayohusiana na usafiri wa Anga.
Mkufunzi wa Chuo cha Usafiri wa Anga Tanzania Aristid Kanje akitoa mafunzo juu ya kozi mbalimbali zinazotolewa na chuo cha Usafiri wa Anga(CATC),wakati Kongamano la siku moja la maadhimisho ya siku Usafiri wa anga Duniani yaliyofanyika makao makuu ya (TCAA) Ukonga Banana jijini Dar es Salaam. Lengo kuu la kongamano hilo ilikuwa ni kuwahamasisha wanafunzi hao wapende masomo yanayohusiana na usafiri wa Anga.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...