Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni, Mhandisi Hamad Masauni akizungumza na wachezaji wa Timu ya Mpira wa Miguu, Miembeni Club kabla ya timu hiyo kupambana na Timu ya Taifa Jang’ombe katika Uwanja wa Amani, Zanzibar. Masauni aliwaambia wachezaji wa Timu hiyo inayotoka katika Jimbo lake, wajitume na wahakikishe ushinde unapatikana. Hata hivyo timu hizo zilitoka sare kwa kufungana goli moja kwa moja.Picha na MOHA.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni, Mhandisi Hamad Masauni (kushoto aliyevaa kofia) akiwa na Katibu wa Timu ya Miembeni, Simai Mwalimu wakiingia ndani ya Uwanja wa Amani, Zanzibar kwa ajili ya kushuhudia timu hiyo inayotoka katika Jimbo la Masauni, ikipambana na Timu ya Taifa Jang’ombe katika mzunguko wa Ligi Kuu visiwani humo.Picha na MOHA.
Mchezaji wa Timu ya Miembeni akipiga mpira kichwa akimtoka mpinzani wake wa Timu ya Taifa Jang’ombe katika mechi ya Ligi Kuu Zanzibar iliyofanyika katika Uwanja wa Amani na Timu hizo zilitoka sare kwa kufungana goli moja kwa moja. Picha na MOHA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...