Na Woinde Shizza,Meru
KAMANDA wa Polisi mkoa wa Arusha, Naibu Kamisha wa Polisi (DCP) Charles Mkumbo amethibitisha kukamatwa kwa mtuhumiwa Wilson Elius anayeshikiliwa kwa kosa la ubakaji lililotokea Novemba 13 eneo la USA River Mkoani Arusha.
Kamanda Mkumbo alimesema kuwa mtuhumiwa alikamatwa kwa rb namba RB/R/4250/2016 na atafikishwa mahakamani upelelezi ukikamilika.
Mwanafunzi huyo wa kidato cha tatu katika shule ya sekondari (imehifadhiwa jina)mkoani Arusha ameshindwa kuendelea na masomo baada ya kubakwa na kutelekezwa kwenye korongo la mchanga .
Akielezea tukio hilo mwanafunzi huyo ambae amehifadhiwa jina kwa sababu za
kimaadili alisema kuwa tukio hilo lilitomkea Novemba 13 majira ya saa 12.30
alipotoka kwa kinyozi.
Alisema kuwa ghafla akiwa anarudi nyumbani alikutana na mtu huyo
aliyemfanyia kitendo hicho na kuanza kumkaba shingoni na kumziba mkono ili
asitoe sauti na ndipo alipomfanyia kitendo hicho cha ukatili ambacho
kimemfanya ashindwe kuendelea na masomo yake vizuri.
"Nilijitahidi sana kupiga kelele ila kutokana na alivyokuwa amenikaba
shingoni alinifanyia kitendo hiki kikatili ambacho kimenipelekea nishindwe
kuendelea na masomo yangu kwani baada ya vipimo nimeonekana aliniumiza
sehemu nyingi ikiwemo hata kifua changu"alisema mwanafunzi huyo.
Kwa upande wa mama mzazi wa mwanafunzi huyo aliyejitambulisha kwa jina la Rambikiaeli
Akyoo alisema kuwa kutokana na vitendo vya ukatili kukithiri kwa mabinti
zao ni vyema serikali ikawa inawachukulia hatua mapema wanaohusika kwani
tangu akamatwe mtuhumiwa huyo na kupelekwa kituoni bado hajasomewa shtaka
linalomkabili hivyo kufanya wanaohusika na vitendo hivyo kuona wako sawa
kwa vile hakuna hatua kali inayochukuliwa mapema dhidi ya matukio hayo
Nae Mkuu wa shule hiyo, Nkoe Nicolaus alisema kuwa tukio hilo limemfanya
mwanafunzi huyo aathirike kisaikolojia kwani tangu afanyiwe ukatili huo
ameshindwa kuendelea na masomo yake vizuri hivyo anawashauri wazazi wa
binti huyo kumuhamisha shule hiyo na kumuhamishia nyingine ili kimbadilisha
mawazo ya kifikra.
Kwa upande wake mwenyekiti wa kitongoji cha kitefu tanesc,o Samweli Matayo
alikiri kutokea kwa tukio hilo katika kitongoji chake na kusema kuwa mara
baada ya taarifa walifanikiwa kumtia hatiani mtuhumiwa aliyetambulika kwa
jina la Wilson Elias ambae ndie aliyehusika na ukatili huo na kumfikisha
katika kituo kidogo cha Polisi Usa River ili kukabiliana na shutuma hizo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...