Katika
kuadhimisha miaka 55 ya Uhuru wa Tanzania Bara tarehe 9 Disemba, 2016 Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania kwa kutumia madaraka aliyopewa chini ya Ibara ya 45(1)(d)
ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ametoa msamaha kwa wafungwa
wafuatao:-
(i)
Wafungwa wote wamepunguziwa
moja ya sita (1/6) ya vifungo vyao zaidi ya punguzo la
kawaida linalotolewa chini ya kifungu 49(1) cha Sheria ya Magereza Sura ya 58
isipokuwa wafungwa walioorodheshwa katika Ibara ya 2 (i-xx).
(ii)
Wafungwa wagonjwa
wenye magonjwa kama UKIMWI, KIFUA KIKUU
(TB) na SARATANI (CANCER) ambao
wako kwenye “terminal stage”.
Wafungwa ambao wamethibitishwa na Jopo la Waganga chini ya Uenyekiti wa Mganga Mkuu wa Mkoa/Mganga Mkuu wa Wilaya.
(iii)
Wafungwa wazee wenye umri wa miaka
sabini (70) au zaidi ambao umri huo umethibitishwa na Jopo la Waganga chini ya
Uenyekiti wa Mganga Mkuu wa Mkoa/Mganga Mkuu
wa Wilaya.
(iv)
Wafungwa wa kike walioingia na mimba
gerezani, pamoja na wale walioingia na watoto wanaonyonya na wasionyonya.
(v)
Wafungwa wenye ulemavu wa mwili na
akili (Physical disability and mental
disability) ambao ulemavu huo umethibitishwa na Jopo la Waganga chini ya
Uenyekiti wa Mganga Mkuu wa Mkoa/Mganga
Mkuu wa Wilaya.
2. Aidha, Msamaha huu wa Mheshimiwa Rais
hautawahusu wafungwa wafuatao:-
(i)
Wafungwa waliohukumiwa adhabu ya
kunyongwa.
(ii)
Wafungwa waliohukumiwa adhabu ya
kunyongwa na adhabu hiyo kubadilishwa kuwa kifungo cha maisha au kifungo
gerezani.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...