theNkoromo Blog, Dar.
SHIRIKISHO
la Vyuo vya Elimu ya Juu-CCM, limemuunga mkono Rais Dk. John Magufuli,
kwa kuamua maadhimisho yajayo ya Uhuru kufanyika Dodoma, likisema uamuzi
huo umedhihirisha dahamira yake ya dhati ya kuhakikisha Dodoma inakuwa
Makao Makuu ya nchi kwa vitendo.
Limemuunga,
Rais Magufuli kwa kuweka wazi katika hotuba yake kwamba Serikali ya
awamu ya tano itaendelea kuchukua hatua kali ikiwa ni pamoja na
kuwatumbua hadharani wale waliozoea kutumbua hadharani mali za
Watanzania na pia kuendelea kuchukua hatua kali katika masuala ya rushwa
na ufisadi, kwa sababu rushwa ni saratani.
Shirikisho
hilo, pia limemuunga Rais kwa tamko lake la hivi karibuni la kuamuru
machinga, wachimbaji wadogo na wafugaji kutofukuzwa hovyo hadi mamlaka
zinazohusika zitakapotenga maeneo maalumu, likisema pongezi hizo ni kwa
sababu Rais amedhihirisha kuwa anajali zaidi masikini na wanyonge.
Salam
hizo zimesemwa leo, Desemba 10, 2016, na Katibu Msaidizi wa CCM, Daniel
Zenda alipozungumza na Waandishi wa habari Ofisini kwake, Makao Makuu
ya Shirikisho la Vyuo vya Elimu ya Juu-CCM, jijini Dar es Salaam, akitoa
taarifa ya Shirikisho hilo kuingiza wanachama wapya 100 toka Chuo Kikuu
cha Tiba na Afya Muhimbili.
"Kwa
kweli tunayo mengi ya kumuunga mkono na kumpongeza Rais, hata hili la
kununua ndege sita. Ndege hizi licha ya kusaidia kurahisisha usafiri wa
anga pia zitasaidia sana kukuza utalii ambao utachangia kuongeza mapato
ya nchi, na ni matarajio yetu mapato yakiongezeka uchumi utakua na hata
bei za bidhaa zitapungua na hivyo Watanzania walio wengi kupata nafuu
ya maisha".
"Pia
sisi kama Watanzania lazima tumuunge mkono na kumpongeza Rais kwa
kuendelea kuonyesha dhamira ya serikali ya awamu ya tano kutoa elimu
bure kwa kitendo chake cha kutenga kila mwezi sh. bilioni 18.777 kwa
ajili ya kutoa elimu bure kwa shule za msingi na sekondari na kwa Vyuo
Vikuu sh. Bilioni 483 kutoka sh. bilioni 340 za mwaka jana, hali ambayo
imewezesha ongezeko la wanafunzi kutoka 98,000 hadi kufikia 125,000
waliojiunga na vyuo vikuu mwaka huu", alisema Zenda.
Akizungumzia
wanachama hao wapya ambao ni madaktari waatarajiwa, katika hafla
iliyofanyika Upanga , Dar es Salaam, Zenda alisema, wakati akiwapokea,
aliwaambia wamefanya vizuri kujiunga na CCM kwa kuwa wamejiunga na chama
makini chenye serikali sikivu inayowajali wanyonge chini ya Rais Dk.
John Magufuli.
Shirikisho
linawa taka wanafunzi hao na Watanzania kwa kujumla kubeza propaganda
zinazosemwa na baadhi ya wanasiasa, kwamba kwa nini ndege zinanunuliwa
wakati hakuna dawa katika hospitali.
"Propaganda
hii ni upotoshaji mkubwa wenye lengo la kutaka kuwafanya Watanzania
hawana akili, maana kila mmoja anajua kwamba katika kipindi hiki kifupi
alichoingia madarakani Rais Dk. Magufuli ameboresha sekta ya afya katika
maeneo mengi ikiwemo upatikanaji wa dawa katika hospitali, zahanati na
vutuo vya afya", Alisema Zenda.
Alisema,
miongoni mwa maboresho aliyofanya Rais kwenye sekta ya afya ni pamoja
na kuongeza bajeti ya sekta hiyo ya afya kwa ajili ya manunuzi ya dawa
kutoka Sh. bilioni 31 hadi kufikia sh. bilioni 250 mwaka huu.
Katibu
Msaidizi wa CCM, Daniel Zenda akizungumza wakati akiwapokea wanachama
wapya 100 wa CCM kutoka Chuo Kikuu cha Muhimbili, katika hafla
iliyofanyika jana, Upanga jinini Dar es Salaam.
Kazi iendelee kunataarifa nyingi za baadhi ya watumishi wasiotimiza wajibu was named kulalamika hasa waliozoea kuibia serikali kwa kulipana posho kodi za waTanzania
ReplyDelete