Mwanza Desemba 1,2016:Kampuni ya TBL Group, leo imezindua Chibuku Super kwenye chupa ya bia ya ml 500, huku ikitoa wito kwa watanzania kutumia vinywaji vinavyozalishwa hapa nchini ili kujenga uchumi wa taifa kwa ujumla.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi huo uliofanyika katika ukumbi wa kiwanda kilichopo eneo la Pasiansi Mwanza , Meneja Masoko wa TBL Group, Bw. Oscar Shelukindo alisema uzinduzi wa bia hiyo ya Chibuku Super” kwenye chupa ya glasi inayorudishwa (Returnable) unatarajiwa kuleta mapinduzi makubwa katika soko la Bia hapa nchini.

“Leo ni siku ya furaha kubwa sana kwetu TBL na kwa watumiaji wote wa Bia yetu hi ya asili , kwani tumeweza kuzindua Bia hii imetengenezwa kwa utaalamu wa hali ya juu na kwa kutumia mitambo ya kisasa kabisa, hivyo kuwahakikishia wanywaji Ubora wa hali ya juu, ina ujazo wa nusu lita na itauzwa kwa bei ya shilingi 700/- tu, kwa chupa na 14,000 kwa kreti,’’ alisema.

Akiizungumzia bia hiyo Shelukindo alisema inatengenezwa kwa kutumia malighafi za hapa nyumbani, ikiwemo nafaka ya mahindi na mtama bora toka kwenye ardhi ya Tanzania na hivyo kutoa kila sababu kwa watanzania kujivunia kinywaji chenye asili ya taifa lao.

“Chibuku Super ina kilevi cha asilimia 4, kinachomfanya mtumiaji aweze kuitumia kwa muda mrefu akiwa na marafiki, lakini pia inampa lishe nzuri kutokana na virutubisho vinavyopatikana katika nafaka zinazotumika kutengeneza bia hii,’’ aliongeza

 Wafanyakazi wa kampuni ya bia ya TBL wakionyesha kwa waandishi wa habari chupa mpya ya Chibuku Super ya Ml 500 wakati wa hfla fupi ya uzinduzi  iliyofanyika jijini Mwanza leo.
 Wafanyakazi wa kampuni ya bia ya TBL wakionja Chibuku super ya Ml 500 wakati wa hfla fupi ya uzinduzi  iliyofanyika jijini Mwanza leo.
Meneja Masoko wa TBL Group Oscar Shelukindo,akizungumza na waandisi wa kuhusiana na  muonekano mpya wa chupa ya Chibuku Super ya Ml 500 wakati wa hafla fupi iliyofanyika jijini Mwanza leo. kulia ni Meneja Kiwanda  cha Chibuku Super Mwanza Herbert Ilembo.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...