Afisa Mawasiliano wa Udart, Deus Buganywa akizungumza na waandishi habari hawapo pichani juu ya utoaji huduma ya usafiri katika jiji la Dar es Salaam, leo.
Abiria wakiwa katika Kituo cha mabasi yaendayo Haraka leo jijini Dar es Salaam.picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii.

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.
Kampuni ya usafiri katika jiji la Dar es Salaam (UDART) imesema kuwa itaendelea kutoa huduma bora ya usafiri kadri ya uwezo wao.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Afisa Mawasiliano wa Udart , Deus Buganywa amesema nia ya kampuni ni kuona wananchi wa jiji la Dar es Salaam wanapata huduma usafiri ulio bora.

Deus amesema kampuni imekuwa ikipokea maoni mbalimbali ya wananchi na kuweza kufanyia kazi katika masuala ua utoaji huduma ya usafiri.

Amesema abiria ni kiungo kikubwa kwao katika kuwasafirisha kutoka sehemu moja na kwenda nyingine bila usumbufu huku mifumo mingine ikiendeleaa kuimarishwa ukiwemo wa matumizi ya kadi.

Aidha amesema wanafunzi sasa wamekuwa na usafiri wa uhakika pasipo kupata unyanyasaji wowote ambao unaweza kufanya achukie shule kutokana na adha ya usafiri.

Amesema mabasi yaliyopo na mahitaji ya abiria hayatoshi wataendelea kuongeza ili wananchi kuwa na uhakika wa safari zao na kuweza kuleta maendeleo ya nchi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...