Serikali imeondoa kaya 55, 692 katika Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini (TASAF), Awamu ya tatu kutokana na sababu mbalimbali. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) amesema hayo leo jijini Dar es salaam.

“Sababu za kuondolewa kwa kaya hizo ni kifo, kuhama kijiji/mtaa ambapo mpango haujaanza kutekelezwa, kutojitokeza mara tatu mfulululizo kupokea ruzuku, mnufaika kuwa mjumbe wa kamati mbalimbali za mpango, wastaafu, viongozi wa watumishi wa Umma.” Waziri Kairuki alisema na kuongeza hilo lilibainika baada ya uhakiki alioagiza kufanyika mwezi Februari, 2016.
Waziri Kairuki alisema katika uhakiki huo kaya zilizokuwa na mwanakaya aliyefariki au wote kufariki zilikuwa 13, 898, kaya zilizohama vijiji/mitaa ambapo mpango haujaanza kutekelezwa 6,228. Aliongeza kaya ambazo hazikujitokeza mara tatu mfululizo kupokea ruzuku zilikuwa 17,746, zilizothibitishwa kuwa sio masikini zilikuwa 13,468 na kaya zilizogundulika kuwa na baadhi ya wanakaya wajumbe wa kamati za usimamizi za Jamii, Halmashauri za Vijiji/Kamati za Mitaa, Viongozi na watendaji zilikuwa 4,352.
Mhe. Kairuki aliainisha kuwa kufuatia agizo lake alilotoa mwanzoni mwa mwaka huu hadi Septemba 2016 kiasi cha shilingi 6,427,110,309 kimeokolewa kwa kaya 42, 035 zilizoondolewa kwa kipindi hicho, na kusisitiza kiasi hicho kitaongezeka kwasababu zoezi hilo linaendelea.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) akisisitiza jambo kwa Waandishi wa Habari kuhusu Kaya zilizoondolewa kwenye Mpango wa kunusuru Kaya Masikini katika Awamu ya Tatu ya TASAF Tatu kwa kukosa sifa.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) akizungumza na Vyombo vya Habari jijini Dar es Salaam kuhusu Kaya zilizoondolewa kwenye Mpango wa kunusuru Kaya Masikini (TASAF), Awamu ya Tatu kwa kukosa sifa. Kushoto kwake ni Katibu Mkuu, Ikulu, Bw. Peter Ilomo na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bi. Susan Mlawi.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...