Mkuu wa Bidhaa wa Vodacom Tanzania, Samson Mwongela (kushoto) akisaidiwa na Meneja Uhusiano kampuni hiyo, Matina Nkurlu (katikati), kuonyesha simu feki zilizokusanywa kutoka kwa wateja wao kwa ajili ya kuteketeza kama ilivyoagizwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), wakati  wa mkutano wa waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo.Kulia ni Gideon Chilambo ambaye ni  Mkurugenzi wa  kampuni ya Chilambo General Trade Company inayoteketeza bidhaa feki.
Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania, Matina Nkurlu (katikati) akionyesha simu halisi aina ya Smart Prime 7 yenye ubora na kiwango inayouzwa kwa Tsh 250,000/-, wakati akizungumza  na  waandishi wa habari juu ya simu feki zilizokusanywa na kampuni yake kutoka kwa wateja kwa ajili ya kuteketezwa kama ilivyoagizwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), jijini Dar es Salaam leo. Kushoto ni Mkuu wa Bidhaa wa kampuni hiyo, Samson Mwongela na kulia ni Gideon Chilambo ambaye ni  Mkurugenzi wa  kampuni ya Chilambo General Trade Company inayoteketeza bidhaa feki.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...