WAZIRI
wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Mazingira na Muungano Mh. January
Makamba amesema kuwa mpango wa serikali ni kuwa na vyanzo vingi vya
uzalishaji umeme ili kuwa na vyanzo vya nchi endelevu na kuunga mkono
juhudi za benki ya dunia kuzalisha umeme wa upepo katika nchi
zinazoendelea ikiwemo Tanzania.
Makamba
amesema hayo wakati wa Kongamano la wadau wa Nishati ya umeme
walipokutana kuzungumzia matumizi ya Nishati ya umeme inayozalishwa kwa
njia ya upepo itakayounganishwa kwenye gridi ya taifa na mfumo huo
utawasaidia wananchi wa Singida .
"Kwa
kuwa umeme huo utazalishwa kwenye maeneo ya vijijini, wananchi
wanatakiwa kupata umeme kwa bei rahisi kulingana na uchumi wao na sio
kuuziwa umeme kwa bei juu, na zaidi Wizara yake inapenda kuweka wazi
kuwa huu mradi una faida kubwa sana kulingana na mfumo wa nchi
ulivyo,"amesema Makamba.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Kampuni ya kuzalisha umeme wa upepo Afrika Mashariki Six
Telecoms, Rashid Shamte amessema kuwa mfumo huu wa gridi ndogondogo una
faida kubwa sana kwa wananchi kwani asilimia kubwa kulingana na ripoti
ya benki ya dunia wananunua umeme wa bei nafuu kwahiyo serikali
imekubaliana na kampuni yetu na imeweza kukubali kuwa mradi huu una
tija na utasimamiwa na serikali yenyewe kupitia kwa Mkuu wa Mkoa wa
Singida pamoja na Halmashauri.
Shamte
ameendelea na kusema, kwa Phase ya kwanza watatoa umeme megawati 100 na
itaendelea mpaka kufika megawati 300 na wataunganisha kwenye gridi ya
taifa, na huu mradi utakuwa na faida kwa wananchi pamoja na wale
watakaotolewa kwenye maeneo yao watafaidika kwa kulipa stahiki zao.
Kwa
upande wa Wizara ya Nishati na Madini, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya
Nishati na Madini anayeshughulikia Nishati, Dkt. Juliana Pallangyo
amewataka wawekezaji hao kuuza umeme kwa bei rahisi kwani mara nyingi
mipango ya serikali imekuwa haiendani na mikakati ya wawekezaji kwahiyo
wanategemea kuona kuwa mradi huu uwe nafuu ya wananchi wa vijijini
kupata umeme kwa bei rahisi.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais - Mazingira na Muungano Mheshimiwa January Makamba akizungumza kwenye mkutano wa wadau wa umeme kujadili mkakati ya kuzalisha nishati ya Umeme kwa njia ya Upepo leo katika ukumbi wa Hotel ya Hyatt Jijini Dar.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...