Na Hassan Mabuye 
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Makazi Mhe. William Lukuvi (pichani)  amevifutia hatimiliki viwanja 15 vilivyokuwa vinamilikiwa na raia mmoja wa Uingereza ambapo serikali imevitaifisha viwanja hivyo vilivyopo katika mikoa ya kanda ya ziwa.
Viwanja hivyo vilivyokuwa vinamilikiwa na Mfanyabiashara maarufu jijini hapa, Hermant  Patel, mwenye uraia wa Tanzania na Uingereza kitendo ambacho ni kinyume na taratibu na sheria za nchini zinazozuia raia wa kigeni kumiliki ardhi.
Aidha, Mhe. Lukuvi amesema anayeruhusiwa kumiliki ardhi nchini ni raia wa Tanzania pekee na kuongeza kwamba kwa watanzania waishio nje ya nchi na kuukana uraia wao nao hawataruhusiwa kumiliki ardhi bali watapewa ardhi kama ilivyo kwa wawekezaji kutoka mataifa mengine.
Mhe. William Lukuvi amesema mtu akishaukana uraia wa Tanzania hana haki tena kama raia wa Tanzania, hivyo ataruhusiwa kumiliki ardhi kama mwekezaji tu na siyo kama raia wa Tanzania. 
Mhe. Lukuvi amesisitiza kuwa ardhi itabaki kuwa ya Watanzania tu na ameagiza mamlaka zota kutawasaka wale wote ambao wanamiliki ardhi kinyume na sheria za nchi.
Uamuzi wa kufuta hatimiliki hizo ulitolewa na Waziri Lukuvi wakati akizungumza na wanahabari juu ya hatua hiyo ya Serikali ya kuvifuta hati hizo jijini Mwanza. 
Lukuvi alisema kuwa awali Serikali ilikuwa ikifahamu mfanyabiashara huyo ana hatimiliki ya viwanja vitano lakini baada ya uchunguzi uliohusisha Taasisi ya Kuzia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) mkoani Mwanza wamebaini raia huyo anamiliki jumla ya viwanja 15.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...