Dokta HARRISON MWAKYEMBE.

Waziri wa Katiba na Sheria, Dokta HARRISON MWAKYEMBE, ametoa ufafanuzi kuhusu uteuzi wa Rais JOHN MAGUFULI wa Wabunge Wawili, pamoja na Naibu Waziri kuteuliwa kuwa Balozi, huku akisisitza kuwa Katiba ya Jamhuri ya Muungano haijakiukwa.
          Akizungumza na Uhuru Fm, Waziri MWAKYEMBE, ameshangazwa na baadhi ya watu kushutumu teuzi hizo za Wabunge wa kuteuliwa alizofanya Rais, huku akisema Katiba ya Nchi inampa nafasi Rais kuteua na kutengua nafasi ya mtu yoyote aliyemteua.
          Amesema ni vema watanzania wakamuacha Rais afanyekazi zake ikiwemo kufanya teuzi kwa kuwa yeye ndiye anaona mtu gani anafaa wapi na nani amteue kwa wakati gani.
          


      Jana jioni, Rais JOHN MAGUFULI, amemteua Dokta ABDALLAH POSSI kuwa Balozi, ambaye Kituo chake cha kazi na tarehe ya kuapishwa itatangazwa baadae.  
          Kabla ya uteuzi huo Dokta POSSI alikuwa Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu aliyekuwa akishughulikia Ulemavu.
    Kwa mujibu wa Waziri MWAKYEMBE, Ubunge wa Kuteuliwa wa Dokta POSSI unakoma kufuatia uteuzi huo wa kuwa Balozi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...