Na  Bashir  Yakub.

Hivi karibuni kumeibuka  miradi  mingi  binafsi  na  ya  serikali   hasa kupitia  NHC ya  ujenzi  wa  nyumba   za  pamoja. Miradi ipo  kwa  majina  tofauti  ipo  inayoitwa APARTMENT, CITY,  VILLAGE,  TOWN, n.k. Baadhi  ipo  kigamboni,  Arusha  na  maeneo  mengine .

 Pia  ipo  katika  mitindo  tofauti  ipo  ile  ya  maghorofa   ya  kwenda  juu, maghorofa  ya mshazali,  na  ile  ya  nyumba  moja  moja   lakini  katika  eneo  moja (common ground).  

Kutokana  na  hilo  makala yalenga kukufahamisha  usinunue  tu  kwa kupenda  muonekano,mazingira  na  rangi , bali  pia uwe  na  uhakika  wa  faraja(comfortability)  inayotokana  na mambo mengine  nje ya muonekano,  rangi  na  mazingira.

1.TOFAUTI  KATI  YA  NYUMBA  ZA  MIRADI  NA  NYUMBA  ZA  KAWAIDA.

Ipo  tofauti  kati  ya  nyumba  za  kawaida  tulizozoea  na  hizi  za  miradi  zilizotajwa  humu.  Tofauti  ipo  katika ngeli hizi :
( a )   Taratibu  zake  za  ununuzi.
( b )  Vitu  unavotakiwa kujua  kabla   ya  ununuzi.  
( c )   Sheria  zinazozilinda   na,  
( d )  Maisha   yako  baada  ya  kuwa  umenununua.

Makala  yataeleza   vitu  unavyotakiwa  kujua    vinavyotofautisha   nyumba  hizi  na  nyingine za  kawaida.

 2.     VITU  UNAVYOTAKIWA  KUJUA.

( a )   Uwepo  wa  malipo  na  michango  mbalimbali.  Pamoja na  kuwa ni mali  yako umenunua , kanuni  ya  15( 2 )  ya  The  Unit  Title  Regulations, G.N 357/2009  imeeleza   baadhi  ya  michango. Ipo  michango  kwa  ajili  ya  chama  na  uongozi,  michango  kwa  ajili  ya  maeneo  ya  matumizi  ya  pamoja, michango  kwa  ajili  ya  huduma  mbalimbali  mnazotumia  pamoja.  

Michango  hapa haihusishi bili  zako  za  umeme,maji n.k. Michango  hii  inaweza  kuwa  inalipwa  kila  mwezi   au  vinginevyo   kadri  ya  utaratibu  wa  eneo  husika.

Hii  ni  tofauti  na  nyumba  za  kawaida  ambazo  haziko  katika  mfumo  huu  ambapo  ukinunua  umenunua  hakuna  mchango  wa  chama  au  vinginevyo.

BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...