Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kulia) akimkaribisha
Mkuu wa Mahakama ya Umoja wa Mataifa (UNMICT), Ofisi ya Arusha, Samwel Akorimo
wakati viongozi wa Mahakama hiyo walipomtembelea kiongozi huyo wa Wizara, ofisini kwake,
jijini Dar es Salaam leo, kwa lengo la kujadili masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya
UNMICT na Wizara hiyo. Katikati ni Msajili wa Mahakama hiyo, Dk. Elias Olufemi.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kulia) akizungumza na
Mkuu wa Mahakama ya Umoja wa Mataifa (UNMICT), Ofisi ya Arusha, Samwel Akorimo
(wapili kushoto) na Msajili wa Mahakama hiyo, Dk. Elias Olufemi (kushoto), wakati
walipomtembelea Wizarani kwa lengo la kujadili masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya
UNMICT na Wizara hiyo.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kushoto) akimsikiliza
Mkuu wa Mahakama ya Umoja wa Mataifa (UNMICT), Ofisi ya Arusha, Samwel Akorimo
(kulia) wakati alipokuwa akifafanua jambo kuhusiana na masuala mbalimbali ya ushirikiano kati
ya UNMICT na Wizara hiyo. Wapili kulia ni Msajili wa Mahakama hiyo, Dk. Elias Olufemi.
Mazungumzo hayo yalifanyika ofisini kwa Naibu Waziri, jijini Dar es Salaam leo.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (watatu kulia), Mkuu wa
Mahakama ya Umoja wa Mataifa (UNMICT), Ofisi ya Arusha, Samwel Akorimo (wapili kulia),
Msajili wa Mahakama hiyo, Dk. Elias Olufemi (watatu kushoto), wakiwa katika picha ya pamoja
na maafisa wengine mara baada ya Mhandisi Masauni kufanya mazungumzo na ujumbe huo,
ofisini kwake, jijini Dar es Salaam leo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...