Serikali wilayani Handeni imepiga marufuku uuzaji holela wa mkaa ili kudhibiti matumizi mabaya ya rasilimali za misitu NA kuwataka wananchi kutumia vituo rasmi kuuza na kununua mkaa. 

Marufuku hiyo ilitolewa na Mkuu wa wilaya ya Handeni Mh. Godwin Gondwe alipokuwa akizindua vituo maalumu vilivyotengwa kwaajili ya kuuzia mkaa (mkaa centre) vinavyotarajiwa kuwa mazingira rafiki kwa vijana wanojihusisha na biashara za mikaa wilayani hapa. 

Mh Gondwe alisema "ni marufuku kuanzia sasa mtu yeyote kuuza mikaa kwenye maeneo ambayo sio vituo rasmi, mkaaa utauzwa na kununuliwa kwenye vituo vilivyopangwa atakayekiuka hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake”. Aliongeza kuwa lengo kuu la kuweka vituo vya kuuzia mkaa ni kudhibiti matumizi mabaya ya rasilimali za misitu; Kulingana na sera ya ukusanyaji mapato,kwa kutumia vituo hivi serikali itaweza kupata mapato yake ambayo hapo awali kulikua na utoroshaji na ukwepaji wa kulipa kodi kwa wavunaji na wauzaji wa mikaa.

Mkuu wa wilaya aliwataka wavunaji wa mkaa kuunda vikundi ambavyo vitawatambulisha na kusaidia kuwa na umoja utakaopelekea kupata vibali halali vya uvunaji wa mazao ya misitu. Alisema kuwa utaratibu huo utasaidia kuwepo kwa uvunaji endelevu ambao utahusisha kupanda miti na kuvuna tofauti na ilivyokuwa awali watu wanavuna miti bila kupanda miti mingine ili kufidia ile iliyovunwa hali itakayoiepusha Handeni kuwa jangwa na kuharibu vyanzo vya maji.

Aliwaeleza wananchi kuwa vituo hivyo vitasaidia kuwa na bei elekezi ambayo itawanufaisha wafanyabiashara wote tofauti na awali ambapo kulikua na ushindani mkubwa uliopelekea wengine kujaza lumbesa ili kupata wateja kwa haraka. 
Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh. Godwin Gondwe na wataalamu wakipata maelekezo mafupi juu ya moja ya kituo cha kuuzia mkaa cha Manga.

Mkurugenzi akionesha baadhi ya vibakuli vilivyokamatwa ambavyo vilitengenezwa na mti aina ya mkarambati tayari kwa kusafirisha kuelekea nchini Kenya kwa mauzo.
Meneja wa wakala wa Misitu Tanzania wa Wilaya ya Handeni akizungumza na wafanyabiashara wa mazao ya misitu ya Mkaa wakati wa Uzinduzi.
Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi Mtendaji Bw. William Makufwe na Meneja wa wakala wa Misitu wa Wilaya Bw. Elias Mwaijere wakitoka kuzindua kituo cha wauza mkaa cha Manga
Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh. Godwin Gondwe akizungumza na wafanyabiashara wa mkaa wakati wa Uzinduzi . 
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Bw. William Makufwe akizungumza na wafanyabiashara wa Mkaa.

Alda sadango,Afisa habari 
Halmashauri ya Wilaya ya Handeni.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...