Aliyekuwa meneja wa wema Martin Kadinda akiwa katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es salaam pamoja na wanasheria
Na Humphrey
Shao,
Globu ya Jamii
Mbunifu wa mitindo
maarufiu nchini, Martin Kadinda amesema kuwa yeye sio meneja wa msanii Wema Sepetu kwa
sasa bali amefika mahakamani hapo kama rafiki wa karibu wa msanii huyo.
Kadinda amesema
hayo katika maongezi maalum na mwandishi huyu juu ya uhusiano wake
na Wema Sepetu kwa sasa hasa mara baada ya kuhusishwa na tuhuma za matumizi na
uuzwaji wa dawa za kulevya.
“Kwa sasa
mie sio meneja wa Wema.K wa sasa mimi ni rafiki yangu tu wa karibu hivyo
nimeamua kuja hapa kwa ajili ya kujua rafiki yangu amefikia wapi katika kipindi
hiki ambacho anapitia magumu” amesema Kadinda
Amesema kuwa
yeye kwa sasa anaendelea na biashara yake ya kushona suti tu hili aweze
kujipatia ugali wake wa kila siku na sio kujihusisha na makundi ambayo sio
sahihi.
Kadinda na marafiki kadhaa wa Wema wameonekana mahakamani hapo wakisubiri kwa hamu kumuona rafiki yao anafikishwa hapo lakini hakufikishwa kama ilivyoelezwa awali.
Baadhi ya marafiki wa Wema Spetu wakiwa wamesimama kusubiri msanii huyo kuletwa mahakamani
Jike Shupa na wenzie wakiwa wamekata tamaa mara baada ya kuambiwa Wema haletwi mahakamani
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...