Meya Isaya ametoa kauli hiyo jiji hapa leo wakati wa maulidi ya kusherehekea kuzaliwa kwa Mtume wao Muhammad Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam ambapo pamoja na mambo mengine amesema kwama jiji la Dar es Salaam bila dua za waze, mashehe na viongozi wote wadini huwezi kuliongoza kutokana na changamoto zilizopo. 

“ Najua changamoto zilizopo kenye jiji hili ni nyingi wazee wangu naomba mnisaidie sana, peke yangu siwezi, dua zenu na ushauri wenu ndio unaweza kunisaidia mimi kufanya mambo mazuri” na wananchi wakaishi kwenye mazingira wanayopenda” amesema Meya Isaya.

Leo hi mimi nikiwa na kiburi kweu kwa ajili ya madaraka haya ambayo nyie ndio mlionipa, sitaweza kutatua changamoto hata moja,zipo changamoto za kimiundombinu ya elimu, na nyingine, ambazo zote zinahitaji kupatiwa ufumbuzi, nawaombeni saa waze wangu mnipe baraka zenu” aliongeza.

Akizungumzia suala la maadili Meya Isaya amesema wazazi hawana budi kuwasaidia walimu, serikali na viongozi kwa ajili ya malezi bora hususani wakiwa shuleni.

Amesema ni jambo la ajabu na mtihani mkubwa kwa walimu ikiwa mzazi atakuwa mstari wa mbele kumnunulia mwanae simu hali yakuwa yupo masomoni jambo ambalo linafanya ashindwe kuzingatia masomo na badala yake kushinda kwenye mitanda ya kijami.

Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam,Isaya Mwita,akisalimiana na Mwenyeji wake,Daluwesh Dume (katikati) kwenye hafla ya sherehe ya Maulid ya Mtume S.A.W iliyofanyika Mtaa wa Da Estate eneo la Kinondoni jijini Dar es Salaam leo. 

Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam,Isaya Mwita,akizungumza katika hafla ya ufunguzi wa sherehe ya Maulid ya Mtume Mohamed S.A.W iliyoandaliwa na Muumini wa Dini hiyo Daluwesh Dume iliyofanyika Mtaa wa Ada Estate eneo la Kinondoni jijini Dar es Salaam leo. Katikati ni Diwani wa Kata ya Kinondoni,Mustapha Muro. 

Meya wa Jiji la Dar es Salaam,Isaya Mwita akiwa na Diwani wa Kata ya Kinondoni,Mustapha Muro wakifuatilia kwa umakini sherehe hizo.
Kikundi cha Al Farouq kikipiga dufu wakati wa sherehe ya Maulid ya Mtume Mohamed S.A.W iliyoandaliwa na Muumini wa Dini hiyo Daluwesh Dume iliyofanyika Mtaa wa Da Estate eneo la Kinondoni jijini Dar es Salaam leo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...