Na Humphrey Shao, Globu Ya Jamii

Kocha msaidizi wa klabu ya Yanga, Juma Mwambusi amekiri kuwa timu yake ilikuwa na tatizo katika eneo la ukabaji na kupelekea kuchapwa bao 2-1.

Mwambusi amesema hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kumalizika kwa mchezo huo na kuelezaa ubovu wa timu yake.

“tulianza mchezo huu vizuri lakini tatizo la ukabaji katika timu yetu ndio limetugharimu na kuwapa wapinzani wetu ushindi wa wazi ambao kila mtu ameuona” amesema Mwambusi.

Mwambusi ametaja kuwa kulikuwa hakuna sababu ya timu yao kupoteza mchezo huo kwani tayari walikuwa washatangulia kwa bao moja hivyo walikuwa na nafasi nzuri ya kupata ushindi lakini uzembe wa wachezaji wachache umeigharimu timu.

Ametaja kuwa tatizo lililowakumba wapinzani wao la kupewa kadi Nyekundu, lilikuwa zawadi tosha ya kuondoka na ushindi lakini bado wachezaji walishindwa kukaba.
Kocha msaidizi wa yanga Juma Mwambusi akiwa na kocha mkuu wa timu hiyo George Rwandamina wakipanga jambo katika mchezo wao dhidi ya Simba.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...