Na Stella Kalinga, SIMIYU
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza
la Mapinduzi, Mhe.Dkt.Ali Mohamed Shein ametimiza ahadi ya kutoa sadaka ya
vifaa vya ujenzi wa Msikiti wa MASJID RAUDHAL mjini Bariadi, ambao ni
Msikiti mkuu Simiyu.
Rais Shein alitoa ahadi hiyo mwezi
Oktoba 2016 wakati alipokuwa Mkoani Simiyu kuwaongoza Watanzania katika
Maadhimisho ya Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru, Wiki ya Vijana na Kumbukumbu
ya Kifo cha Baba wa Taifa Mwl.Nyerere.
Akizungumza wakati wa makabidhiano ya
vifaa hivyo,Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony Mtaka amemshukuru Mhe.Rais Shein
na kubainisha kuwa ujio wake mwaka jana umeleta mafanikio makubwa kwa mkoa na
kujenga uhusiano mazuri kati ya Mkoa wa Simiyu na Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar.
Mtaka amesema ujio wa Dkt Shein mkoani
Simiyu umefungua milango ya ushirikiano wa kibiashara kati na Zanzibar, ambapo
alimtuma Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali, Mhe.Riziki Pembe Juma mwezi Desemba
mwaka jana kuja kuona Chaki za Maswa na sasa Mkoa huo unauza chaki Zanzibar.
Mkuu
wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka(wa tatu kushoto) na Sheikh Mkuu wa Mkoa
huo,Mahamoud Kalokola (wa nne kushoto) na viongozi wengine wa BAKWATA mkoa
wakipokea baadhi ya vifaa vya ujenzi vilivyotolewa na Rais wa
Zanzibar,Mhe.Dkt.Ali Mohamed Shein kukamilisha ujenzi wa msikiti wa MASJID RAUDHAL
mjini Bariadi kutoka kwa mwakilishi wake Ally Habshy Abdallah
Mkuu wa
Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka akizungumza na baadhi ya viongozi wa BAKWATA kabla
ya kupokea vifaa vya ujenzi vilivyotolewa na Rais wa Zanzibar,Mhe.Dkt.Ali
Mohamed Shein ili kukamilisha ujenzi wa msikiti wa MASJID RAUDHAL mjini Bariadi kutoka kwa
mwakilishi wake Ally Habshy Abdallah.
Sheikh wa
Mkoa wa Simiyu, Mahamoud Kalokola akizungumza na baadhi ya viongozi wa BAKWATA
kabla ya kupokea vifaa vya ujenzi vilivyotolewa na Rais wa Zanzibar,Mhe.Dkt.Ali
Mohamed Shein ili kukamilisha ujenzi wa msikiti wa MASJID RAUDHAL mjini Bariadi kutoka kwa
mwakilishi wake Ally Habshy Abdallah.
Mwalikishi
wa Rais wa Zanzibar,Mhe.Dkt.Ali Mohamed Shein Ndg. Ally Habshy Abdallah
akizungumza viongozi
wa BAKWATA kabla ya kuwasilisha vifaa vya ujenzi alivyovitoa kama sadaka yake
ili kukamilisha ujenzi wa msikiti wa MASJID RAUDHAL mjini Bariadi.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,
Mhe.Anthony Mtaka akagana na baadhi ya
viongozi wa BAKWATA mara baada ya makabidhiano ya vifaa vya ujenzi wa Msikiti wa MASJID RAUDHAL mjini Bariadi
kutoka kwa Rais wa
Zanzibar,Mhe.Dkt.Ali Mohamed Shein.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...