Wagonjwa wa Satarani wanaotibiwa katika taasisi ya Uchunguzi wa Saratani ya Ocean Road iliyopo jijini Dar es Salaam wataanza kunufaika na huduma bora kwa njia ya kisasa kwa kutumia Teknolojia ya Mawasiliano kutokana na mchakato wa serikali kuimarisha huduma za taasisi hiyo.

Wakati jitihada hizo za serikali zinaendelea sekta baadhi ya sekta binafsi zimeanza kuunga mkono jitihada hizo za serikali ambapo kampuni ya mawasiliano ya Vodacom kupitia taasisi yake ya kuhudumia masuala ya kijamii imetoa msaada wa kompyuta 10 za kisasa kwa taasisi hiyo.

Akiongea wakati wa kupokea msaada huo katika hafla iliyofanyika hospitalini hapo leo,Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi hiyo,Dk.Julius Mwaiselage,amesema kuwa msaada huu umepatikana katika kipindi mwafaka ambapo hospitali hiyo iko katika mchakato wa kuendesha huduma zake kidigitali.
Dk.Mwaiselage alisema kuwa hivi sasa kumekuwepo na ongezeko kubwa la wagonjwa wanaofika hospitalini hapo kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi na kutibiwa hivyo kuna umuhimu mkubwa kuhakikisha kuwa ili kuwahudumia ni kuwa na huduma za kisasa katika kila idara kwa njia ya TEKNOHAMA na tayari serikali na wadau mbalimbali wameanza kufanikisha mchakato huo.

Aliishikuru kampuni ya Vodacom kwa kuwa mstari wa mbele kuunga mkono jitihada hizo “Tunawashukuru Vodacom Tanzania Foundation kwa kuunga mkono jitihada za kuboresha huduma zetu ili ziweze kuwa bora zaidi na tunatoa wito kwa taasisi nyingine kuendelea kutuunga mkono katika mapambano haya ya kutokomeza ugonjwa wa Saratani nchini na kuwapatia huduma bora wahanga wa ugonjwa huu”.Alisema.
 Wafanyakazi wa Vodacom Tanzania  wakiwa na misaada mbalimbali  kwa ajili ya wagonjwa wanaopata  matibabu   katika Taasisi ya Uchunguzi wa Saratani ya Ocean Road jijini Dar es Salaam  wakati walipowasilia kwenye taasisi hiyo  hivi karubni  kutoa msaada   wa kompyuta 10 za kisasa kwa taasisi hiyo kupitia kitengo chake cha Vodacom Tanzania Foundation. Msaada huo utarahisiha utoaji wa huduma bora kwa angonjwa.
 Mkuu wa Kitengo cha  Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom,Tanzania  Jacqueline Materu (kulia) na Mkurugenzi wa mawasilianao wa Wizara ya ujenzi ,Uchukuzi na Mawasiliano ,Mhandisi  Clarence Ichwekeleza (Kushoto) wakimsikiliza kwa makini  Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Uchunguzi wa Saratani ya Ocean Road jijini Dar es Salaam  ,Dk.Julius Mwaiselage, wakati alipokuwa akishukuru kwa Taasisi ya  Vodacom Tanzania Foundation  kwa  kuwapatia msaada wa Kompyuta 10 za kisasa  kwa ajili ya kusaidia kutao huduma bora kwa wagonjwa wanaotibiwa katika Taasisi hiyo mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.

 Mkuu wa Kitengo cha  Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom,Tanzania  Jacqueline Materu (kulia) , Mkurugenzi wa mawasilianao wa Wizara ya ujenzi ,Uchukuzi na Mawasiliano ,Mhandisi  Clarence Ichwekeleza (wapila kulia )  na Meneja ruzuku na Mawasiliano wa Vodacom Foundation Sandra Osward,  (wapili kushoto) wakimpongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Uchunguzi wa Saratani ya Ocean Road jijini Dar es Salaam  ,Dk.Julius Mwaiselage,(kushoto) wakati alipokuwa akiwaonyesha waandishi wa habari (hawapo pichani) moja ya  Komputa  kati ya 10 za kisas alizopewa msaada na Taaisi ya Vodacom Tanzania Foundation , kwa ajili ya kusaidia kutao huduma bora kwa wagonjwa wanaotibia katika Taasisi hiyo mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Kitengo cha  Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom,Tanzania  Jacqueline Materu (kulia) akimkabidhi Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Uchunguzi wa Saratani ya Ocean Road jijini Dar es Salaam  ,Dk.Julius Mwaiselage,(kushoto)  moja ya kompyuta kati ya 10 za kisasa zilizotolewa msaada na Taasisi ya Vodacom Tanzania Foundation  kwa ajili ya kusaidia kutao huduma bora kwa wagonjwa wanaotibiwa katika Taasisi hiyo mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
'
Wanaoshuhudia ni Mkurugenzi wa mawasilianao wa Wizara ya ujenzi ,Uchukuzi na Mawasiliano ,Mhandisi  Clarence Ichwekeleza (wapili kulia) na Meneja ruzuku na Mawasiliano wa Vodacom Foundation Sandra Osward.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...