Mbio za Kili marathon zimefanyika leo manispaa ya Moshi mjini
mkoani Kilimanjaro katika viwanja vya chuo cha ushirika ambapo
wakimbiaji zaidi ya 8000 wameshiriki mbio hizo.
Mbio hizo zimefunguliwa rasmi na Katibu Mkuu wa Wizara
ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Prof. Elisante Ole Gabriel
majira ya saa kumi na mbili nusu asubuhi ambapo mbio za kilometa 42
zilianza, huku wale kilometa 21 wakianza mbio hizo majira ya saa moja
kamili asubuh.
Mbio hizo ziligawanyika katika makundi tofauti totauti
kuanzia wale waliokimbia umbali wa kilometa 42, umbali wa km 21 huku
kwa upande wa walemavu wao walishindana katika mbio za umbali wa km 10
pamoja na zile za kilometa 5 ambazo hazina ushindani. kila kundi
walipatikana washindi wa mbio hizo.
Washiriki wa Mbio za 21 Km wakiwa tayari kuanza kushindana katika Mbio za Kilimanjaro Marathon 2017, zilizofanyika katika viwanja vya Chuo cha Ushirika, Mjini Moshi Mkoani Kilimanjaro leo.
Sehemu ya Washiriki wa Mbio za 21 KM wakichuana vikalia katika moja ya njia zao mapema leo asubuhi.
Mshiriki wa kwanza kuwasili uwanjani kwa wale walioshiriki mbio za kilomita 42 kwa upande wa wanaume, Moses Mongick ambaye ni raia kutoka nchini Kenya akionyesha furaha yake.
Mshiriki wa kwanza kuwasili uwanjani kwa wale walioshiriki mbio za kilomita 42 kwa upande wa wanawake, Shemith Nyamwira Muriuk kutoka Kenya akiwasili uwanjani huku akiwa ni mwenye furaha tele.
Mshindi wa mbio za kilometa 21 ambaye ni raia wa Tanzania Emmanuel Giniki akiwasili uwanjani.
Mshiriki wa kwanza kuwasili uwanjani kwa wale walioshiriki mbio za kilomita 21 kwa upande wa wanawake, Grace Kimanzi kutoka Kenya akiwasili uwanjani.
Mwanamitindo wa Kimataifa, Miriam Odemba alikuwa ni mmoja wa washirikiwa wa Mbio za kilometa 21.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...