Na,Abel Daud-Globu ya Jamii Kigoma.

Wakati Serikali ya Jamuhuri ya muungano wa Tanzania ikiunga mkono juhudi zinazofanywa na Asasi,Makanisa,Mashirika na watu binafsi,wamisionari wa kanisa la Baptist kutoka Marekani wameunga mkono juhudi za serikali kwa kujenga jengo la wodi ya watoto katika hospitali teule ya Manispaa ya Kigoma Ujiji lenye thamani ya shilingi milion 420.

Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Samson Anga-akizindua jengo hilo ameupongeza uongozi wa kanisa hilo na kusema kuwa serikali inaendelea kuchukua hatua ili kumaliza changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya afya,ikiwa ni pamoja na kuwataka wakazi wa kigoma kutumia jengo hilo vizuri na kupata huduma zitakazotolewa ili kuimalisha afya za watoto.

Aidha akisoma risala ya uzinduzi wa jengo hilo katibu wa Hospitali teule ya Manispaa ya kigoma ujiji Bw.Anania Raiton ameeleza kuwa bado kuna changamoto nyingi katika sekta ya afya,na kuongeza kuwa kama serikali itachukua hatua katika kumaliza changamoti hizo za huduma itakayo kuwa inatolewa kwa uma,itasaidia kuokoa maisha ya wahitaji wa matibabu.

Hata hivyo kwa upande wao wafadhili wa jengo hilo akiwemo Dr.Larry Pepper ambaye ni mwakilishi wa wafadhili katika hospitali ya Baptist ameeleza kuwa gharama zilizotumika ni kubwa,hivyo ametoa wito kwa wakazi wa Mkoa wa Kigoma kutumia huduma vizuri ikiwa ni pamoja na kuepuka kuharibu vifaa ambayo vitatumika kutolea huduma.

Kwa upande wake Mganga Mfawidhi wa Hospital ya Baptist Kilawa Shido amesema kuwa kuwepo sasa kwa jengo hilo,wakazi wa Kigoma watarajie kunufaika sambamba na kutoa shukurani kwa wafadhili,huku akiitaka serikali kuongeza wahudumu katika sekta ya afya kwani uhitaji wao ni mkubwa mno.

Pichani kati ni Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Samson Anga akikata utepe kuashiria uzinduzi jengo la wodi ya watoto katika hospitali teule ya Manispaa ya Kigoma Ujiji lenye thamani ya shilingi milion 420.
Baadhi ya Vitanda hivyo vilivyomo ndani ya wodi ya watoto .

Mganga Mfawidhi wa Hospital ya Baptist Kilawa Shido akimuelezea Mkuu wa Wilaya Samson Anga jinsi kifaa hicho kitakavyokuwa kinafanya kazi.

Baadhi ya Vitanda vingine vilivyomo wodini humo.

Jengo la wodi ya watoto lililozinduliwa .


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...