Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.
Dr. John Pombe Joseph Magufuli amewapandisha cheo Maafisa sita wa Uhamiaji kuwa
Makamishna wa Uhamiaji kuanzia tarehe 28
mwezi Februari mwaka 2017, Wakati huo huo amewateua kushika nyadhifa
mbalimbali katika Jeshi la Uhamiaji.
Walioteuliwa kushika nyadhifa hizo ni Mrakibu
wa Uhamiaji (SI) Edward Peter Chogero kuwa Kamishna wa Divisheni ya Fedha na
Utawala, Mrakibu Mwandamizi wa Uhamiaji (SSI) Samwel Rhobby Magweiga kuwa
Kamishna wa Divisheni ya Udhibiti na Uongozi wa Mipaka, Mrakibu Mwandamizi (SSI)
wa Uhamiaji Gerald John Kihinga kuwa Kamishna wa Divisheni ya Pasipoti na
Uraia, Mrakibu Mwandamizi wa Uhamiaji (SSI) Musanga Mbusuro Etimba kuwa
Kamishna wa Divisheni ya Hati za Ukaazi na Pasi, Mrakibu Mwandamizi wa Uhamiaji
(SSI) Hannerole Morgan Manyanga kuwa Kamishna wa Divisheni ya Sheria.
Aidha Mh.Rais amemteua pia Naibu Kamishna wa
Uhamiaji Mourice David Kitinusa kuwa Kamishna Chuo cha Uhamiaji cha Kikanda (TRITA).
Uteuzi huo unaanzia tarehe 28 mwezi
Februari mwaka 2017.
Imetolewa na
Meja Jenerali Projest
Rwegasira
Katibu Mkuu
Wizara ya Mambo ya Ndani ya
Nchi
26 Machi 2017
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...