KUZ: 27.01.1943 – KUF:
28.03.2016
Leo tarehe 28 Machi, 2017
umetimiza mwaka mmoja kutoka ulipotuacha na kwenda kwa Muumba wako. Hatuna
maneno yanayoweza kuelezea majonzi na huzuni ya kuagana nawe lakini kumbukumbu
yako itaishi nasi siku zote.
Tunakumbuka upendo wako usio na ubaguzi, utu wako
na ukarimu wako ambao ulimfanya kila aliyekufahamu kuguswa kipekee.
Tunamshukuru mwenyezi Mungu
kwa kutujalia kuwa na mama kama wewe kwa
muda wote tulioishi nawe hapa duniani. Unakumbukwa daima na mume wako mpenzi Mzee
Stephen Philip Assey, watoto wako ,wajukuu zako, majirani zako, ndugu, jamaa na
marafiki.
Misa ya kumwombea
marehemu mama yetu mpendwa itafanyika katika Kanisa Katoliki la Mt Martin
De Porres lililopo Mwananyamala tarehe 2
Aprili 2017, saa 3.00 kamili asubuhi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...