Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii

Mfuko wa Pensheni wa LAPF umeanza kuandikisha wanachama kutoka sekta na serikalini za binafsi na ongezeko hilo imetokana na wanachama kutumia fursa ya kuchagua mfuko ulio sahihi wenye ubora .

Akizungumza leo na Waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Meneja Mafao wa LAPF , Ramadhani Mkeyenge amesema pamoja na kuwepo kwa huduma hiyo mfuko umeboresha huduma za ulipaji wa mafao kwa wakati.

‘’ Mwanachama wa LAPF anaekaribia kustaafu hutaarifiwa mapema ili kujiandaa kwa kuwa na nyaraka zote zinazohitajika na hulipwa siku moja kabla ya kustaafu’’.

Mkeyenge ameongeza kuwa kwa mwaka 2015\2016 mfuko wa Pensheni umeweza kulipa kiasi cha bilioni 107 kwa wanachama wake huku kipindi cha mwaka 2011\2012 mfuko ulifanikiwa kulipa kiasi cha shilingi bilioni 38.1 kwa wanachama hii ilitokana na ongezeko la wanachama.

‘’Mwaka 2015\2016 wanachama 316 wamepewa mikopo kiasi cha bilioni 10.5 ambapo hadi kufikia sasa LAPF ina wanachama zaidi ya 165,000’’.aliongeza Mkeyenge.

Mfuko wa Pensheni umekuwa ukiwahudumia wanachama wake kwa takribani zaidi ya miaka 70 na mafao ambayo yanatolewa ni pamoja na pensheni ya uzee,warithi,ulemavu,mikopo ya elimu pamoja na pensheni ya kujitoa.
Meneja Mafao wa LAPF , Ramadhani Mkeyenge akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya LAPF inavyofanya kazi kwa wanachama leo jijini Dar es Salaam,kulia ni Afisa Matekelezo Mwandamizi LAPF, Katiti Katiti.picha na Emmanuel Mssaka,Globu ya jamii.
Afisa Matekelezo Mwandamizi LAPF, Katiti Katiti akizungumza na waandishi wa habari juu ya LAPF inavyofanya kazi kwa wanachama wake, leo jijini Dar es Salaam.kushoto ni Meneja Mafao wa LAPF , Ramadhani Mkeyenge
Baadhi ya Wanahabari wakifuatilia mkutano huo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...