Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauniakizungumza na Maafisa na Askari wa vyombo vya Ulinzi na Usalama vilivyo chini ya Wizara yake, katika Ukumbi wa Bwalo la Magereza, mjini Kilwa mkoani Lindi. Masauni aliwataka maafisa na askari hao kuongeza nguvu zaidi katika ukamataji wa wahamiajiharamu pamoja na wauza dawa za kulevya. 
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (katikati), akiwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi, Renatha Mzinga (kushoto) wakati Naibu Waziri huyo alipokuwa anakagua Makazi ya askari Polisi, Mitwero mkoani humo ambapo nyumba za askari hao zimechangaa na chache kutokana na wingi wa askari hao. Hata hivyo, Serikali hivi karibuni inatarajia kujenga nyumba mpya katika eneo hilo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi, Renatha Mzinga akimuonyesha Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni eneola Mitwero mkoani humo ambalo nyumba za makazi ya askari polisi zitakapojengwa. Masauni alikagua nyumba wanazoishi askari hao kwasasa pamoja na kukagua eneo hilo makazi mapya yatakapojengwa. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...