Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Mhe. Jaji (R) Semistocles Kaijage amewataka watumishi wa tume hiyo wazingatie maadili na kanuni za utawala bora ili kutekeleza kwa ufanisi jukumu la Tume katika kukuza na kuimarisha demkorasi na utawala bora nchini.
Jaji Kaijage ameyasema hayo alipoalikwa kuwa mgeni rasmi kufungua kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Tume kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima jijini Dar es Salaam.
“Jukumu kubwa la Tume ni kukuza na kuimarisha demkorasi na utawala bora nchini, kwa maana hiyo ni muhimu kwamba watumishi wa Tume wazingatie maadili na kanuni za utawala bora ili kutekeleza kwa ufanisi jukumu hili” alisema na kuongeza kuwa:
“Ni muhimu kwa watumishi wa Tume katika utendaji kazi wao kuepuka vitendo vya ukiukwaji wa maadili kama vile rushwa, upendeleo na au ubaguzi wa aina yoyote katika sehemu ya kazi”
Mbali na hayo, Mhe. Jaji Kaijage aliipongeza Tume kufanikisha uchaguzi mdogo uliofanyika mwezi Januari mwaka huu katika jimbo la Dimani na kata 20 za Tanzania Bara kwa kuufanya kuwa wa amani na utulivu pamoja na changamoto mbalimbali zilizoukabili uchaguzi huo.

Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi  wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) ambaye ni Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Bw. Kailima Ramadhani akimkaribisha Mgeni Rasmi wa Ufunguzi wa Kikao cha baraza hilo ambaye ni Mwenyekiti wa NEC Mhe. Jaji (R) Semistocles Kaijage baada ya kuwasili kwenye viwanja vya Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima jijini Dar es Salaam ambako kikao hicho kilifanyika.Kushoto ni Katibu Mkuu wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali na Afya Tanzania (TUGHE) Taifa Bw. Heri Mkunda.
 Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Bw. Kailima Ramadhani (aliyesimama) akitoa neno la ukaribisho kwa Mgeni Rasmi wa ufunguzi wa Kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Tume hiyo Mhe. Jaji (R) Semistocles Kaijage (kulia kwake) kabla ya kufungua kikao hicho.Kulia ni Katibu Mkuu wa (Tughe) Taifa Bw. Heri Mkunda na kushoto ni Katibu wa Baraza hilo Bi. Rose Malo. 
Mgeni Rasmi Mhe. Jaji (R) Semistocles Kaijage akizungumza na wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Tume (hawapo pichani) kabla ya kufungua kikao hicho kwenye ukumbi wa mikutano wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima jijini Dar es Salaam.Kushoto kwake ni Mwenyekiti wa Baraza Bw. Kailima Ramadhani, Katibu Mkuu wa Tughe Taifa Heri Mkunda na kulia kwake ni Katibu wa Baraza hilo Bi. Rose Malo na Naibu Katibu Bi. Uddy Sadick. 

Katibu Mkuu wa Tughe Taifa        Bw. Heri Mkunda (kulia) akitoa neno la shukrani kwa Mgeni Rasmi wa Kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Mhe. Jaji (R) Semistocles Kaijage (kushoto).Katikati ni Mwenyekiti wa baraza hilo Bw. Kailima Ramadhani 
 
 Katibu wa Baraza la Wafanyakazi  wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi  Bi. Rose Malo akiwasilisha muhtasari wa kikao kilichopita cha baraza hilo huku Mwenyekiti wa Baraza Bw. Kailima Ramadhani (katikati) na Naibu Katibu Msaidizi Bi Uddy Sadiki wakifuatilia muhtasari wa kikao hicho.
Kwa taarifa kamili BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...