Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii

Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini limetoa ratiba ya michezo miwili ya Kombe la Shirikisho maarufu kama Azam Sports Federations Cup (ASFC) kwa timu za Yanga na Azam ambazo zilikuwa hazijapangwa.
Mechi hizo zilishindikana kuchezwa baada ya Yanga na Azam kuwa wawakilisji katika michuano ya kimataifa ambapo April 95 Azam itashuka dimbani kuvaana na Ndanda kwenye Uwanja wa Azam Complex Chamazi.
Yanga ambao bado wanaendelea kuiwakilisha nchi kwenye kombe la Shirikisho barani Afrika wao mchezo wao utakuwa April 22 watakapovaana na Tanzania Prisons kwenye Uwanja wa Taifa.
Taarifa kutoka TFF zimesema kwamba michezo miwili ya mwisho ya Robo Fainali za ASFC zimepangiwa tarehe na pazia la nane bora litafungwa Aprili 22.
Tayari Simba ya Dar es Salaam na Mbao FC ya Mwanza zimekwishafuzu hatua ya Nusu Fainali baada ya kuzitoa Kagera Sugar ya Bukoba na Madini FC ya Arusha katika Robo Fainali.
Mbao FC iliwafunga Kagera Sugar 2-1 Uwanja wa Kaitaba, Bukoba wakati Simba SC iliwafunga Madini FC 1-0 Uwanja wa Sheikh Amri Abeid mjini Arusha bao pekee la Mrundi, Laudit Mavugo.
Kikosi cha Prisons FC
Kikosi cha Yanga

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...