Na Fadhili Atick Globu ya Jamii Mbeya

 Mkuu wa mkoa wa Mbeya Amos Makala amefanya mkutano wa hadhara wa kusikiliza kero za wananchi mtaa wa Shewa kata ya Mwakibete mkoani Mbeya,na kuwataka wananchi kushirikiana na serikali katika kutatua Changamoto mbalimbali zinazo wakabili.

Makala ambaye ametembelea Shule ya Msingi Shewa na kushuhudia msongamano wa wanafunzi,  amepongeza wananchi kwa kushiriki ujenzi wa madarasa kupunguza msongamano wa wanafunzi, ambapo halmashauri ya jiji la Mbeya walichangia shilingi milioni 6.3 kuunga Mkono jitihada za wananchi.

Makala ameahidi kufuatilia kwa Karibu ujenzi wa madarasa mpaka yakamilike, kwani wananchi wamekuwa wakichukizwa na baadhi ya watu wachache wanaopita kushawishi wananchi wasichangie

Makala amewaonya wote wanaoshawishi wananchi kutochangia Maendeleo kuacha tabia hiyo mara moja katika  na kuamua kuonyesha mfano wa kuchangia milioni moja katika ujenzi wa choo cha Shule msingi shewa

Pia ameagiza Tanesco na Mamlaka ya Maji kushughulikia haraka matatizo ya  Umeme na Maji katika mkoa wa Mbeya hili kupunguza kero kwa Wananchi.
 Rc Makalla akizungumza na wananchi wa kata ya mwakibete jijini mbeya
Akishangazwa na wingi wa wanafunzi katika shule ya msingi mwakibete ambapo idadi ilionesha wanafunzi ni wengi kuliko madarasa.
Moja kati ya Wakazi wa shewa kata ya mwakibete wakitoa kero zao mbele ya Mkuu wa mkoa wa Mbeya.
Mmoja wa Wananchi akitoa duku duku lake kwa RC Makala.
Baadhi ya wakazi wa Mwakibete wakifuatilia mkutano huo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...