MWIMBAJI wa kimataifa wa nyimbo za injili, Pastor Solly Mahalangu kutoka nchini Afrika Kusini, amethibitisha kushiriki Tamasha la Pasaka linaloadhimisha miaka 17 tangu kuasisiwa kwake mwaka 2000 chini ya uratibu wa kampuni ya Msama Promotions.

Solly ambaye amekuwa king’ara vilivyo katika muziki wa injili kama mwimbaji anayejipambanua na wengine kama mchangamshaji zaidi jukwaani, pia ni kiongozi wa kanisa nchini Afrika Kusini , hivyo kuenfesha huduma zote mbili kila moja kwa wakati wake.

Alex Msama, Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Tamasha hilo litakalozinduliwa April 16, mwaka huu katika Uwanja wa Uhuru, jijini Dar es Salaam kabla ya kuelekea katika mikoa mingine mitano, alisema jana kwamba mwimbaji huyo amethibitisha kushiriki tukio hilo lenye kubeba hadhi na vionjo vya kimataifa.

“Nikiwa Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Tamasha la Pasaka, nina furaha kubwa kusema kuwa mwimbaji wa kimataifa wa nyimbo za injili kutoka nchini Afrika Kusini, amethibitisha kushiriki tamasha la Pasaka la mwaka huu litakalofanyika katika mikoa sita ikiwemo Dar es Salaam,” alisema.

Alisema ujio wa Mahlangu katika tamasha hilo, kunafanya maandalizi ya Tamasha hilo yazidi kuimarika kutokana na umaarufu wa mwimbaji huyo anayesifika ndani na nje ya Afrika Kusini kwa huduma ya uimbaji wa nyimbo zenye ujumbe wa kuvutia wengi na kuchangamsha jukwaa.

Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya Tamasha la Pasaka, Alex Msama, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, kuhusu maandalizi ya tamasha hilo litakalofanyika Aprili 16 kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam. 
Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya Tamasha la Pasaka, Alex Msama, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, kuhusu maandalizi ya tamasha hilo litakalofanyika Aprili 16 kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam. 


KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...